Hizbollah
-
Tukio la “Iran Moyo Mmoja”:
Sheikh Naeem Qassem: Iran Daima Iko Kando ya Muqawama / Mmekuwa Mfano kwa Dunia Nzima
Sheikh Qassem pia aliipongeza Iran ya Kiislamu kwa kusimama kwake kwa ushujaa mkubwa dhidi ya uvamizi wa Marekani na Israel kwa kipindi cha siku kumi na mbili, akisema: “Alhamdulillah, mmeonyesha mfano kwa dunia nzima jinsi ya kupambana na uvamizi, kusimama imara, na kufikia mafanikio makubwa kwa baraka za uongozi wa Imam Khamenei (h.a), umoja wa watu na uaminifu wa wanajeshi wenu shupavu. Ushindi huu utaandikwa katika historia.” Akaongeza kwa kusisitiza: “Tunajua Iran inalipa gharama kubwa kwa kusimama upande wa haki, upande wa muqawama, upande wa Palestina, na upande wa mataifa yote yanayohitaji msaada. Lakini hii ndiyo Iran — mfano wa kujitolea, utukufu na uadilifu — ambayo haidai chochote kwa kusimama na wanyonge. Iran hii imesimama kwa ajili ya utukufu wa ubinadamu.” Sheikh Qassem alizungumzia pia vikwazo vipya dhidi ya Iran, akisema: “Leo tena wameiwekea Iran vikwazo vipya. Je, vikwazo hivi viliwahi kuacha kuwepo? Tangu ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu miaka 46 iliyopita, Iran imeendelea kuwa chini ya vikwazo, lakini kila siku taifa hili limeendelea kung’aa zaidi na kuthibitisha kuwa ni taifa la ukweli na la mapambano.”
-
Yemen katika Macho na Moyo wa Sayyid Hassan Nasrallah katika Miaka 11 ya Mapinduzi ya Yemen
Watu wa Yemen katika kumbukumbu ya miaka 11 ya ushindi wa Mapinduzi yao wanapanga kufanya maadhimisho ya kumbukumbu ya Sayyid wa Muqawama, kwa kuwa uhusiano wa Sayyid Muqawama na wananchi pamoja na viongozi wa Yemen ulikuwa ni uhusiano wa pande mbili uliojaa mapenzi na heshima.
-
Maandamano Makubwa ya Wenyeji Lebanon Kupinga Uamuzi wa Serikali wa Kuvunja Silaha za Muqawama
Wananchi wa maeneo mbalimbali ya Lebanon wamefanya maandamano na mikutano ya hadhara kupinga uamuzi wa serikali wa kuhodhi na kuvunja silaha za vikosi vya Muqawama.
-
Abdulmalik al-Houthi: Mpango wa Kuvinyang’anya Silaha Vikundi vya Muqawama ni wa Kipuuzi na Unahudumia Maadui
“Lau Umma wa Kiislamu ungetilia mkazo tangu mwanzo juu ya ujenzi wa jeshi la Kipalestina lenye nguvu, hali ya leo isingekuwa kama ilivyo.”
-
Msimamo Mkali wa Hizbullah Dhidi ya Jaribio la Kuvunjwa kwa Silaha za Muqawama: Azimio Jipya la Serikali ya Nawaf Salam ni Tishio kwa Uhuru wa Lebanon
Chama cha Hizbullah kimetoa tamko kali kupinga uamuzi mpya wa serikali inayoongozwa na Nawaf Salam, ambao wanauona kama hatua ya hatari ya kudhoofisha muqawama (mapambano ya ukombozi) na kukabidhi usalama wa Lebanon kwa Marekani na utawala wa Kizayuni wa Israel. Katika taarifa hiyo, Hizbullah imesisitiza kuwa itakabiliana na uamuzi huu kwa msimamo thabiti kama hatua isiyokubalika kabisa, huku ikisisitiza umuhimu wa kulinda silaha za kujihami na kuimarisha jeshi la taifa kwa ajili ya kutetea ardhi na uhuru wa Lebanon. Lebanon Bado Chini ya Vitisho vya Israel na Marekani