Ishara
-
Mamilioni ya Waumini Washuhudia Mbele ya Mwenyezi Mungu Wema wa Kiongozi Shahidi Kupitia Sala ya Maiti
Mamilioni ya waumini walioshiriki katika mazishi ya Ayatullah Mkuu Sayyid Ali Husseini Khamenei walimwombea dua katika Sala ya Maiti, wakimshuhudia mbele ya Mwenyezi Mungu kuwa alikuwa mja mwema na kumuombea rehema na daraja ya juu.
-
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya: Iran Haitaruhusu Uingiliaji wa Usimamizi wa Mlango wa Bahari wa Hormuz
Makao Makuu ya Khatam al-Anbiya (s) yametangaza kuwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran haitaruhusu kwa hali yoyote uingiliaji wa mamlaka yoyote katika usimamizi wa Mlango wa Bahari wa Hormuz, huku yakiahidi kutoa jibu kali dhidi ya kile ilichokitaja kuwa uchokozi wa Marekani.
-
Ujumbe wa Wanazuoni wa Palestina Wawasili Iran Kutoa Heshima kwa Mwili Msafi wa Shahidi aliyeishi kwa kutetea Quds na Watu wa Palestina
Ujumbe wa masheikh na wanazuoni kutoka Palestina umewasili Jamhuri ya Kiislamu ya Iran kwa ajili ya kutoa heshima na kuonesha mshikamano wao kwa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran na Kiongozi Mkuu wa Iran Shahidi Sayyid Ali Khamenei (ra); huku ukisisitiza nafasi ya Kiongozi huyo wa Mapinduzi ya Kiislamu katika kuunga mkono Quds Tukufu na haki za wananchi wa Palestina.
-
Bendera ya Maombolezo ya Imam Hussain (AS) Yapandishwa katika Haram ya Hazrat Fatimah Masoumeh kuukaribisha Mwezi wa Muharram
Mamia ya Mazuwwari na wakazi wa mji wa Qom walishiriki hafla ya kupandisha Bendera Nyeusi ya maombolezo ya Imam Hussein (AS) juu ya Kuba la Haram ya Hazrat Fatimah Masoumeh (SA), kuashiria kuanza kwa Mwezi Mtukufu wa Muharram na kumbukumbu ya Mashahidi wa Karbala.
-
Radiamali Ilhan Omar Kuhusu Tukio la Ukatili Dhidi ya Mwanamke Muislamu Wakati wa Hotuba ya Trump
Mbunge Muislamu wa Marekani Ilhan Omar alilaani kukamatwa kwa mmoja wa wageni aliyehudhuria hotuba ya Donald Trump katika Bunge la Marekani, baada ya kushika ishara ya maandamano au kupinga. Omar alisisitiza kuwa hatua hiyo ilikuwa kinyume na haki za kiraia na uhuru wa maoni, na kuhamasisha kulinda nafasi za kila mtu kushiriki kwa amani katika mijadala ya kisiasa bila hofu ya mateso au ukatili.
-
-
Operesheni ya Kisaikolojia huko Karbala: Uchambuzi wa Kihabari wa Ujumbe wa Imam Hussein (a.s) kabla na baada ya Ashura
Mapinduzi ya Imam Hussein (a.s) hayakuwa vita vya kijeshi pekee; bali yalikuwa vita kamili vya kihabari na kisaikolojia vilivyolenga nyoyo na akili za watu. Kuanzia mahubiri ya Makka hadi ujumbe ulioandikwa kwa damu huko Karbala, Imam Hussein (a.s) aliwezaje kuhamasisha maoni ya umma dhidi ya utawala wa Yazid? Uchambuzi wa mkakati wa mawasiliano wa Imam (a.s) katika mojawapo ya nyakati nyeti zaidi katika historia ya Kishia, unaonesha mfano wa kipekee wa uanaharakati wa kihabari unaosimama juu ya ukweli.
-
Tanga | Sheikh Mkuu wa T.I.C Sheikh H. Jalala Mwakindenge Aongoza Hafla ya Ndoa za Vijana 100 Katika Maadhimisho ya Mazazi ya Bibi Fatima Zahra (a.s)
Hafla hii imeendelea kuwa ishara ya umoja, upendo na kuenzi Sunna ya ndoa katika Uislamu, sambamba na kuadhimisha tukio tukufu la mazazi ya Bibi Fatima Zahra (s.a).
-
Picha kuhusu mradi wa fani ya ushonaji kwa ajili ya Palestina katika Msikiti wa Afrika Kusini
Baadhi ya wanaharakati na wafuasi wa Palestina nchini Afrika Kusini wanashona vipande vya kitambaa vyenye rangi za bendera ya Palestina, kuunda kazi ya ishara ya kumbukumbu kwa watoto waliopoteza maisha katika vita vya Ghaza. Kazi hii itafunguliwa rasmi mnamo tarehe 29 Novemba, Siku ya Kimataifa ya Umoja na Palestina.
-
-
Hezbollah: Uhalifu wa Wavamizi Dhidi ya Yemen Unaonesha Kiwango cha Kufilisika Kwao
Hezbollah imetoa tamko likisema kuwa: "Uhalifu na mashambulizi yanayofanywa na wavamizi (yaani utawala wa Kizayuni wa Israel) dhidi ya Yemen ni ishara ya wazi ya kufilisika kwao kisiasa, kiakhlaqi na kijeshi."