Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Katika mkutano na Spika na Wabunge wa Bunge la Kiislamu la Iran, Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Ali Khamenei, amesema kwamba: "Iran Haijawahi Kuyumba Mbele ya Mashinikizo ya Kimataifa".
Aliendelea kusisitiza juu ya:
1- Msimamo Usioyumba wa Taifa la Iran dhidi ya madola makubwa duniani, akisema kuwa huo ni ishara ya wazi ya uwezo na dhamira ya kitaifa.
2- Wito kwa Wabunge: Amewahimiza Wabunge kuhifadhi heshima na nafasi ya kipekee ya Bunge la Kiislamu na kuepuka hatua zozote zinazoweza kudhoofisha taasisi hiyo muhimu.
3- Umoja na M shikamano: Alionya kuhusu majaribio ya maadui kuleta migawanyiko ndani ya Iran na akaeleza kuwa wabunge wanapaswa kuwa makini, waungane na kulinda maslahi ya taifa.
4- Umuhimu wa maadili ya Mapinduzi: Alikumbusha wabunge kuzingatia daima malengo ya Mapinduzi ya Kiislamu na kuepuka kupotoka kwenye njia ya haki na maadili.
Your Comment