Wakati serikali ya muda ya Taliban imetangaza kuwa Gavana wa Mkoa wa Bamiyan, Mawlawi Abdullah Sarhadi, alifika haraka eneo la tukio na kuongoza operesheni ya kuzima moto wa misitu kama ishara ya kujali mazingira, ripoti nyingine zimeripoti uhamishaji wa lazima wa makumi ya familia za Kishia na jamii ya Wahazara kwa amri ya kiongozi huyo huyo wa Taliban – jambo lililosababisha hasira na taharuki kubwa miongoni mwa wananchi na wanaharakati wa kiraia.
Tunafundishwa Dua hii:
اللَّهُمَّ اجْبُرْ كَسْرَ قَلْبِي، وَصَبِّرْنِي عَلَى مَا فَاتَنِي...
"Ewe Mwenyezi Mungu! Tibu moyo wangu uliovunjika, nivumilishe juu ya kilichonipita..."
Kwa Dua hii unajielekeza kwa Allah (SWT) kama Mponyaji wa nyoyo zilizovunjika na Mtulizaji wa roho zilizochoka. Inafundisha kumkabidhi Allah maumivu ya moyo, kukubali kuwa si kila tulichokitaka ni chema kwetu, na kumuomba Atuchagulie kilicho bora.