Khutba
-
Sehemu ya Tatu:
Khutba ya Mtume Mtukufu (s.a.w.w) katika kukaribia Mwezi wa Ramadhani - Sehemu ya Khutba ya Sha‘baniyyah
Katika Mwezi Mtukufu wa Ramadhani, dua za waumini hupokelewa haraka. Ni wakati wa kuomba kwa moyo safi na nia thabiti, hasa kuomba Mwenyezi Mungu atupatie neema ya kufunga Ramadhani na kusoma Qur’ani. Huu ni mwaliko wa kiroho wa kujijenga, kujisafisha na kuimarisha uhusiano wetu na Mwenyezi Mungu.
-
Andiko Kamili la Khutba ya Fadak ya Bibi Fātima Zahra (a.s) pamoja na tarjama yake
1. Mwanzo wa Khutba – Malalamiko kuhusu dhulma na msimamo wa watu Kisha hamkungoja hata kidogo ili moyo uliokuwa umejeruhiwa utulie, na hali ile ngumu iwe nyepesi. Bali mliongeza kuni kwenye moto, mkaufukuzia upepo ili uongezeke kuwaka. Mlikuwa tayari kuitikia mwito wa Shetani, mkijiandaa kuzima nuru angavu ya dini ya Mwenyezi Mungu, na kuondoa Sunna za Mtume Muhammad (s.a.w.w) aliyechaguliwa. Kwa kisingizio cha maslahi, mlikuwa mkila kijuujuu na kuficha nia zenu. Mlikuwa mkifanya njama nyuma ya vilima na miti dhidi ya familia yake na watoto wake. Na sisi tulipaswa kustahimili mambo haya yenye uchungu kama kisu chenye makali makali, au mkuki unaopenya tumboni.
-
Infografia | Utambulisho wa Qā’im wa Aal Muhammad (s.a.w.w) katika Khutba ya Ghadir (9)
"Tambueni! Hakika mwisho wa Maimamu kutoka kwetu ni Qā’im al-Mahdi...Hakika yeye ndiye Hujja aliyebakia, na baada yake hakuna hujja mwingine".
-
Sheikh Hemed Jalala | Khutba ya Ijumaa (Malezi ya Watoto) - Masjidul Ghadir, Kigogo Post, Dar-es-Salaam
Sheikh Hemed Jalala alisisitiza umuhimu wa malezi bora ya watoto kwa kufuata misingi thabiti ya Kiislamu. Alibainisha kuwa familia ni msingi wa jamii, na hivyo malezi ya mtoto yanapaswa kuakisi maadili na mafundisho ya dini.
-
Sheikh Abdul Ghani Khatibu | Khutba ya Ijumaa: “Karama na Heshima ya Mwanadamu - Msimamo Wetu wa Kiutu”
Lengo letu si mkate - Bali ni kuishi kwa hadhi, kwa karama, kwa ujasiri wa kusimamia ukweli, hata kama ni mchungu. Tusimame na wanyonge: Tusisahau ndugu zetu wanaodhulumiwa, kama Wapalestina, ambao kila siku wanapigania si mkate - bali heshima yao, ardhi yao, utu wao na Karama yao.