Kuanza
-
Vyombo vya Habari vya Kiarabu Vyaupa Uzito Ujumbe wa Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu; Vasisitiza Ulipizaji wa Damu na Kuendelea kwa Muqawama
Vyombo vya habari mashuhuri vya eneo hilo kutoka Lebanon, Iraq, Yemen, Palestina, Qatar na Saudi Arabia, vimeripoti kwa upana ujumbe wa Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, uliotolewa baada ya kumalizika kwa ibada kubwa ya mazishi ya Kiongozi huyo aliyefariki akiwa shahidi. Vyombo hivyo vimeutaja ujumbe huo kuwa ni ishara ya kuanza kwa hatua mpya katika uongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu. Miongoni mwa mambo makuu yaliyoangaziwa katika taarifa hizo ni pamoja na kusifiwa kwa ushiriki wa kihistoria wa wananchi, uhusiano kati ya Mapinduzi ya Kiislamu na harakati ya Ashura, kuendelea kwa mbele ya Muqawama (upinzani dhidi ya dhuluma), pamoja na kusisitizwa kwa ulipizaji wa damu za mashahidi wa vita vya hivi karibuni.
-
Aliyekuwa Amir wa Qatar, Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani, afariki dunia akiwa na umri wa miaka 74
Aliyekuwa Amir wa Qatar na Baba Amir, Sheikh Hamad bin Khalifa Al Thani, amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 74, kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa na Amiri Diwan ya Qatar. Sababu ya kifo haijatangazwa.
-
Bendera ya Maombolezo ya Imam Hussain (AS) Yapandishwa katika Haram ya Hazrat Fatimah Masoumeh kuukaribisha Mwezi wa Muharram
Mamia ya Mazuwwari na wakazi wa mji wa Qom walishiriki hafla ya kupandisha Bendera Nyeusi ya maombolezo ya Imam Hussein (AS) juu ya Kuba la Haram ya Hazrat Fatimah Masoumeh (SA), kuashiria kuanza kwa Mwezi Mtukufu wa Muharram na kumbukumbu ya Mashahidi wa Karbala.
-
Ghalibaf Atoa Ujumbe Maalumu Katika Maadhimisho ya Siku 100 za Jihadi ya Taifa la Iran
Spika wa Bunge la Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amelipongeza taifa la Iran kwa msimamo wake wa kujitolea na kujitolea kulinda nchi, akisema umoja wa wananchi uliwavunja moyo maadui na kuiwezesha Iran kushinda changamoto kubwa.
-
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran: Bunge la Kiislamu Ni Nguzo Kuu ya Utashi wa Wananchi na Sheria
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kuwa Majlisi ya Shura ya Kiislamu ni kiini cha wananchi na nguzo muhimu ya sheria na utungaji wa sheria, akieleza kuwa taasisi hiyo ina jukumu la msingi katika kutekeleza matakwa ya wananchi ndani ya mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Ripoti ya Vyombo vya Habari vya Kiebrania Kuhusu Madhara ya Vita na Iran: Kuibua Upya Teknolojia Iliyo Potea Kutachukua Miaka
Gazeti la Yedioth Ahronoth linaripoti kuwa vita vya siku 12 dhidi ya Iran vilichukua mipango ya miaka miwili, na baadhi ya teknolojia za siri za Israel ziliharibika, ambapo kuibua upya kunahitaji miaka kadhaa na kuanza upya katika baadhi ya nyanja.
-
Onyo la Financial Times kuhusu athari za mzozo na Iran; hatari ya vifo kwa wanajeshi wa Marekani
Financial Times limeonya kuwa hatua yoyote ya kijeshi ya Marekani dhidi ya Iran inaweza kusababisha vifo vya wanajeshi wa Marekani na kuathiri siasa za ndani pamoja na kampeni ya Donald Trump, huku uwezo wa mashambulizi makali ukitajwa kuwa mdogo na wa muda mfupi.
-
Kuanza kwa kuondoka kwa majeshi ya wavamizi (wa kizayuni) kutoka Ghaza
Baadhi ya maeneo ya Ukanda wa Ghaza yanashuhudia kuondoka kwa hatua kwa hatua kwa majeshi ya utawala wa Kizayuni na kuanza kwa kurejea kwa wakimbizi.