Kulinda
-
Mkuu wa Mahakama ya Iran Asisitiza Umuhimu wa Umoja wa Kitaifa na Kusema Hakuna Tofauti Kuhusu Kulipiza Kisasi Dhidi ya Adui
Mkuu wa Mamlaka ya Mahakama ya Iran, Hojjat al-Islam Gholam-Hossein Mohseni Ejei, amesisitiza umuhimu wa kulinda na kuimarisha umoja wa kitaifa na mshikamano, akiwataka wananchi kuwa macho dhidi ya wachochezi wa fitina, wanaoeneza uvumi na wanafiki.
-
Msemaji wa Serikali ya Iran: Umoja Ndio Urithi Mkuu Aliouacha Imam Shahidi kwa Iran na Ulimwengu wa Kiislamu
Msemaji wa Serikali ya Iran, Fatemeh Mohajerani, amesema kuwa umoja ndio urithi muhimu zaidi aliouacha Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei kwa Iran na ulimwengu wa Kiislamu, akisisitiza kuwa tofauti za maoni hazipaswi kuudhoofisha urithi huo wa thamani.
-
IRGC Yatangaza Kushambulia Malengo 85 ya Kijeshi ya Marekani kwa Kujibu Mashambulizi ya Marekani
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) limetangaza kuwa limeanzisha hatua ya awali ya kujibu mashambulizi ya Marekani kwa kushambulia malengo 85 ya kijeshi ya Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati kwa kutumia makombora na ndege zisizo na rubani.
-
"Mtu kama mimi hawezi kumpa baia mtu kama yeye" – Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei alipofafanua somo Kubwa la Muharram
Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei alisema kuwa somo kubwa zaidi la Mwezi wa Muharram ni kujitolea kwa Imam Hussein (AS) kwa ajili ya kuilinda dini ya Uislamu, akisisitiza kuwa kila Muumini anapaswa kuwa tayari kujitoa kwa kila alicho nacho pale utetezi wa Uislamu unapohitajika.
-
Muharram 1448H: Wanafunzi Mabinti wa Jamiatul Mustafa Washiriki Majlisi ya Maombolezo katika Msikiti wa Amirul Muuminin (AS), Magomeni
Wanafunzi 144 wa Jamiatul Mustafa, wakiongozana na msimamizi wao, walishiriki majlisi ya maombolezo ya Muharram katika Msikiti wa Amirul Muuminin (AS) uliopo Mgomeni, Dar es Salaam. Majlisi hiyo ilijumuisha muhadhara wa Sheikh Hujjatul Islam wal-Muslimin Aydarus, kisomo cha Qur'ani Tukufu na maombolezo ya Imam Hussein (AS), ikiwa ni sehemu ya kuhuisha ujumbe wa Karbala wa haki, uadilifu na kujitolea katika njia ya Mwenyezi Mungu.
-
Kamanda Mkuu wa Jeshi la Iran: Adui Ametambua Lazima Aheshimu Taifa la Iran na Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu
Jenerali Amir Hatami amesema adui sasa ametambua kuwa hana budi kuheshimu Taifa la Iran na mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu, akisisitiza kuwa msimamo na uthabiti wa wananchi wa Iran umebadili hesabu za wapinzani wao.
-
Jarida la Foreign Affairs: "Uwezo wa Marekani Hautoshi Tena Kutimiza Malengo Yake ya Kimataifa"
Uchambuzi wa jarida la Foreign Affairs unasema kuwa kuongezeka kwa vitisho katika Mlango wa Hormuz na maendeleo ya teknolojia za kijeshi kumeonyesha pengo kati ya matarajio ya kimataifa ya Marekani na uwezo wake halisi wa kudhibiti usalama wa bahari duniani.
-
Ayatollah Nouri Hamedani: Kulinda Umoja wa Kitaifa Ndilo Kipaumbele Kikuu cha Taifa
Marjaa wa Kidini Ayatollah Hussein Nouri Hamedani amesema kuwa kulinda umoja wa kitaifa na kuzuia migawanyiko ni kipaumbele cha juu kwa Iran, huku akisisitiza umuhimu wa kuimarisha huduma kwa wananchi, kujibu ipasavyo uchokozi wa adui na kuendeleza nafasi ya mji wa Qom kama kitovu muhimu cha Kiislamu.
-
Putin Apongeza Siku ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran
Putin ameonyesha kwamba uhusiano kati ya Urusi na Iran ni wa kirafiki na una msingi wa ushirikiano wa karibu. Pia ameahidi kuwa Urusi inaunga mkono Iran katika kulinda udhibiti wake wa ndani, maslahi yake halali, na usalama wake katika mazingira ya kimataifa yenye changamoto.
-
Rais wa Azerbaijan: Hatutumi vikosi vya kulinda amani Gaza
Ilham Aliyev, Rais wa Azerbaijan, ametangaza kuwa nchi yake haina mpango wa kutuma vikosi vyake kushiriki katika operesheni za kulinda amani nje ya mipaka ya nchi, ikiwemo Gaza.
-
Rais wa Baraza la Wahdat Muslimin Pakistan:
Ayatollah Khamenei amewashinda maadui katika kila vita / Wafuasi wa Imam Hussein (a.s) daima wamesimama dhidi ya dhuluma
"Kilichotokea Venezuela ni cha kusikitisha; waziri mkuu wetu amempendekeza mtu apate Tuzo ya Nobel ilhali alihusika katika utekaji nyara wa rais aliyechaguliwa wa nchi hiyo na familia yake. Viongozi wa Pakistan wanapaswa kulaani vikali hatua za Donald Trump. Trump hata alivunja katiba ya nchi yake mwenyewe.”
-
Jukumu la Marajii wa Kidini wa Kishia katika;
"Kulinda Umoja wa Kitaifa na Utambulisho wa Iran / Sehemu ya Saba: Kisa cha Kuokolewa kwa Lugha ya Taifa ya Iran na Ukombozi wa Azarbaijan"
Kulinda umoja wa ardhi na kuzingatia utambulisho wa kidini ni miongoni mwa masuala yaliyokuwa yakipewa umuhimu mkubwa na viongozi wa kidini katika ardhi za Kiislamu. Kiasi kwamba kila aina ya uvamizi au shambulio dhidi ya ardhi za Kiislamu ilikabiliwa na mwitikio mkali kutoka kwao. Uvamiuzi wa Azarbaijan wakati wa Vita vya Pili vya Dunia na juhudi za kuutenga mkoa huo kutoka Iran ni miongoni mwa mambo yaliyodhihirisha tena ushawishi wa uongozi wa kidini katika kulinda umoja wa ardhi ya nchi. Aidha, kulinda utambulisho wa kitaifa wa Kiairani pia lilikuwa ni mojawapo ya masuala yaliyopatiwa umuhimu maalum na viongozi (Marajii) wa kidini katika kipindi cha utawala wa Pahlavi.
-
Kulaaniwa Vikali Shambulio Dhidi ya Katibu Mkuu wa Baraza la Wanazuoni wa Kiislamu wa India katika Mkutano wa Maandamano Mjini Lucknow
Hujjatul-Islam Muhammad Miyan Abidi Qummi: "Lengo kuu la mashambulio kama haya,” alisema, “ni kudhoofisha harakati ya ulinzi wa wakfu na kunyamazisha sauti ya wanaotetea haki.”
-
Nafasi ya Marājiʿ wa Kishia katika Kulinda Umoja wa Ardhi na Utambulisho wa Kitaifa- Sehemu ya 2 | Marāji ni, Walinzi wa Uhuru wa Nchi za Kiislamu
Mfano mashuhuri ni Ayatullah al-Uzma Sayyid Muhammad Hasan Shirazi, ambaye alitoa Fat'wa maarufu ya kupiga marufuku tumbaku mwaka 1891 huko Iran, hatua iliyozuia njama za kikoloni za Waingereza na kuwa alama ya mapambano ya Kiislamu dhidi ya ukoloni. Vivyo hivyo, Ayatullah Kashif al-Ghita, Ayatullah Muhsin al-Hakim, na Imam Khomeini (r.a) walikuwa mstari wa mbele katika kuhimiza mapambano ya kulinda utu, uhuru, na heshima ya mataifa ya Kiislamu.