Madina
-
Msikiti wa Haram ya Imam Reza (a.s) - Mashhad, Iran, Unashikilia Rekodi ya Dunia kwa kuwa na Eneo Kubwa Zaidi Kuliko Misikiti Yote Duniani
Misikiti 10 Yenye Maeneo Makubwa Zaidi Duniani (Tanbihi: Ukubwa unakusudiwa ni Eneo zima la Msikiti - Sio Uwezo wa Idadi ya Waumini wanaingia ndani yake, kwa kutizama uwezo Msikiti wa Kwanza uwezo inakuwa ni Masjid Al-Haram, ndio unaongoza kwa kubeba watu wengi zaidi kuliko Misikiti mingine, kwa Mantiki Masjid Imam Reza a.s inakuwa ya Tatu Duniani kwa kutizama uwezo na Ukubwa wa eneo, lakini inakuwa ya kwanza Duniani kwa kutizama Ukubwa wa eneo tu).
-
Uharibifu wa Makaburi ya Jannat al-Baqi‘ - Historia na Umuhimu Wake
Uharibifu wa Jannat al-Baqii umeacha doa lisilofutika katika historia ya Uislamu. Makaburi haya hayakuwa tu sehemu ya kumbukumbu ya kihistoria, bali pia yalikuwa alama ya mapenzi na heshima kwa watu waliotumikia Uislamu kwa ikhlasi na kujitolea. Leo hii, Waislamu kote duniani wanaendelea kuomba urejesheaji Heshima na Staha inayostahili kwa Makaburi haya matukufu.
-
Hamza(ra), Bendera ya Kwanza ya Uislamu
Hamza bin Abdulmuttalib (ra), ami yake Mtume wa Uislamu(saww), anajulikana kama Bendera ya kwanza ya Uislamu. Kwa ujasiri na kujitolea kwake katika kumtetea Mtume na mafundisho ya Kiislamu, alicheza nafasi muhimu katika kueneza Uislamu. Hamza hakuwa tu shujaa katika uwanja wa vita, bali pia alikuwa mfano na mlinzi wa Waislamu, daima akiwa upande wa Mtume na kwa msimamo wake, alitia nguvu na matumaini katika nyoyo za waumini.
-
Makala Fupi Kuhusu Kuzaliwa kwa Sayyidat Fatima Maasoumeh (sa) | Imam Ridha (as) alisema: "Yeyote atakayemzuru Fatima Maasoumeh Qom, atapata Pepo."
Fatima Maasoumeh (sa) alikuwa mashuhuri kwa elimu yake, ibada, na ufasaha. Alifuatilia harakati za kaka yake, Imam Ridha (as), na alikuwa mstari wa mbele katika kutetea haki na kufichua dhulma za watawala wa wakati huo. Katika safari yake ya kuelekea Khurasan kumtembelea kaka yake aliyehamishwa kwa nguvu na Khalifa Ma’mun, Sayyidat Fatima alifika mji wa Qom (Iran ya leo), ambako alipata maradhi mazito na kufariki dunia tarehe 10 Rabi'ul Thani mwaka 201 Hijria. Alizikwa mjini Qom, ambao baadaye ukawa kituo muhimu cha elimu ya Kiislamu.