Mapenzi
-
Imam Ali (a.s) na Siri za Ukuruba Wake kwa Mtume Mm Muhammad (s.a.w.w)
Imam Ali (a.s) si tu sahaba wa karibu wa Mtume (s.a.w), bali ni zao la malezi ya moja kwa moja ya Mtume, shahidi wa mwanzo wa wahyi, na mhimili wa maadili ya Kiislamu. Upendo na ufuasi wake unabaki kuwa kipimo muhimu cha uaminifu wa kweli kwa Uislamu na Mtume wa Mwenyezi Mungu (s.a.w.w).
-
Nakuru - Kenya | Khatibu wa Sala ya Ijumaa Sheikh Abdul Ghani Khatibu Aeleza Siri ya Utukufu wa Bibi Fatima (sa) kupitia Hadithi Tukufu za Mtume(saww)
Sheikh Abdul Ghani aliweka wazi kuwa mapenzi ya Mtume (saww) kwa Bibi Fatima (sa) hayawezi kuchukuliwa kwa mtazamo wa kawaida wa mapenzi ya baba kwa binti yake. Badala yake, ni tamko la kiungu na kijamii linalobainisha nafasi yake adhimu katika Uislamu.
-
Fadhila za Sayyidat Fatima Zahraa (s.a): Mlinzi Mshikamanifu wa Mtume wa Uislamu (s.a.w.w)
Katika tukio maarufu lililonukuliwa na vitabu vya historia na hadith, Bibi Fatima (a.s) alienda kwa uchungu mkubwa kuondoa matumbo ya ngamia yaliyowekwa na washirikina kichwani mwa Mtume (s.a.w.w) wakati akiwa katika sajda. Tukio hili linabaki kuwa ushahidi wa mapenzi yake ya kipekee na ulinzi usioyumba kwa Mtume wa Uislamu(s.a.w.w).
-
Ustadhi Rajai Ayoub na Wasomi wa Qur'an kutoka Tanzania Wawasili Salama Bangladesh kwa Ajili ya Mahfali Makubwa ya Kimataifa ya Qur'an +Picha
Mahfali hayo ya kimataifa yanakusudiwa kuwa jukwaa muhimu la kiroho na kielimu, ambapo wasomaji bingwa na mahiri wa Qur'an Tukufu kutoka Tanzania watapata fursa ya kuonesha vipaji vyao katika kusoma Aya Tukufu za Mwenyezi Mungu (SWT), kwa mapito na mitindo mbalimbali ya usomaji wa Qur'an (Qira’at).
-
Kiongozi wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan:
"|Leo, yeyote ambaye hayuko pamoja na watu wa Gaza, basi hayuko pamoja na Mungu pia"
Kiongozi wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan, akisisitiza kuwa Marekani na Israel si wa kuaminika wala si marafiki wa Waislamu, aliongeza: Leo, yeyote ambaye hayuko upande wa watu wa Gaza, basi hayuko upande wa Mungu pia.
-
Ziara ya Arubaini ya Imam Hussein (a.s.): Maana na Athari Zake
Ziara ya Arubaini ya Imam Hussein (a.s.) ni shule kamili ya roho, akili, jamii, na siasa. Ni fursa ya kuimarisha imani, kukuza undugu, kupandikiza roho ya kupinga dhulma, na kudumisha kumbukumbu ya kujitolea kwa ajili ya haki. Kuendeleza ibada hii ni njia ya kudumisha maadili ya kimungu na kibinadamu, na kuisambaza kwa vizazi vijavyo.
-
Njia ya Karbala: Safari ya Kiroho Isiyoisha - Kila Hatua ni Mstari wa Mapenzi kwa Hussein (a.s)
Safari ya Arubaini katika Ardhi ya Karbala, inatengeneza Ukaribu wa Kiroho na Hussein (a.s) Katika Kila Hatua unayoipiga ukielekea kumzuru Aba Abdillah Al-Hussein (as).