Msamaha
-
Sheikh Ahmad Haji Atoa Mafunzo Muhimu ya Kujenga Utu na Kukemea Dhulma katika Jamii | "Dhulma huondoa Baraka na Kuleta Majuto"
"Unaweza kumdhulumu mtu na ukalala usingizi mzito, lakini yule uliyemdhulumu halali kamwe. Anakumbuka dhulma yako kila siku na humlalamikia Mwenyezi Mungu dhidi yako. Na ikumbukwe kuwa macho ya Mwenyezi Mungu hayalali,” amesema Sheikh Ahmad Haji, akisisitiza hatari ya dua ya aliyedhulumiwa.
-
-
Masharti na Namna ya Kuswali Swala ya Ijumaa (Swalat Al-Jumu‘ah)
Swala ya Ijumaa ni miongoni mwa ibada zinazotekelezwa kwa jamaah (pamoja na kundi la waumini). Swala hii ina khutba mbili, ambazo huanza kwa kumsifu na kumtukuza Mwenyezi Mungu. Katika khutba hizo, Imamu wa Ijumaa anatakiwa kuwasisitiza watu juu ya taqwa (kumcha Mwenyezi Mungu). Baada ya khutba mbili, swala ya rakaa mbili huswaliwa kama Swala ya Alfajiri, ila kuna tofauti moja muhimu: Katika Swala ya Ijumaa kuna qunut mbili za sunna — moja katika rakaa ya kwanza kabla ya rukuu, na nyingine katika rakaa ya pili baada ya rukuu. Katika kila qunut, mtu anaweza kusoma dua yoyote miongoni mwa zile zinazosomeka katika qunut za swala nyingine, kwa kumwomba Mwenyezi Mungu rehema, msamaha na baraka.