Mtukufu
-
Hujjatul-Islam wal-Muslimin Woldan:
Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni fursa ya Kimungu ya kurekebisha mtindo wa maisha
Mkurugenzi Mkuu wa Tablighi za Kiislamu mkoa wa Fars ameeleza kuwa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani ni fursa ya Kimungu ya kujenga upya roho na kurekebisha mtindo wa maisha. Amesema kuwa Mwenyezi Mungu ameumba mfumo wa uwepo wa mwanadamu kwa namna ambayo katika kipindi fulani cha mwaka huhitaji mabadiliko katika namna ya kuishi na kula; mabadiliko ambayo hupelekea kuinuka kwa roho na kuimarika kwa irada. Ramadhani ni uwanja wa mazoezi ya ibada na kujijenga nafsi, na kwa tafsiri nyingine ni hundi nyeupe yenye saini ya Kimungu kwa ajili ya msamaha na kuangazwa kwa nyoyo.
-
Kikao cha Qur’an katika Husseiniyyah ya Imam Khomeini kikihudhuriwa na Kiongozi Mkuu wa Iran Siku ya Kwanza ya Ramadhan
Kikao cha Qur’an katika Husseiniyyah ya Imam Khomeini (M.A) Siku ya kwanza ya Ramadhan kilisisitiza umuhimu wa Qur’an katika maisha ya kiroho ya Waislamu na thawabu za usomaji wake.
-
Ayatollah Sistani ametangaza kesho (Alhamisi) kuwa ni Siku ya Kwanza ya Ramadhani
Ali al-Sistani ametangaza kuwa kesho Alhamisi ni siku ya Kwanza ya Ramadhani 1447H.
-
Nafasi ya Kupuuzia Mambo ya Kimaada na Thamani za Uongo katika Ndoa
Ndoa ya Bibi Fatima (a.s) na Amirul-Mu’minin Ali (a.s) ni kigezo cha pekee kinachoonyesha jinsi ambavyo mambo ya kimaada na thamani za uongo yalipuuzwa kabisa. Uteuzi wa mwenzi wa maisha ulitokana na taqwa, imani na maadili, si utajiri wala muonekano wa nje. Kwa kuishi kwa urahisi, unyenyekevu na mbali na anasa, walijenga nyumba iliyojaa utulivu, baraka na uimara wa kiroho. Mtindo huu wa maisha unatupa ujumbe wazi: ukombozi kutoka katika pupa ya mali na mapambo ndiyo njia ya kufikia furaha ya kweli katika maisha ya ndoa.
-
Imamu Jamaa wa Zamani wa Masjid al-Haram (Msikiti Mtukufu wa Makkah) Aachiwa Huru Baada ya Miaka 7 Gerezani Saudi Arabia
Sheikh Saleh Al-Talib mnamo mwaka 2018 katika moja ya khutba zake alipinga maonesho ya muziki (konseti) na mikusanyiko ya kijinsia iliyochanganyika, jambo lililosababisha kutoridhishwa na viongozi wa Saudia na pia shinikizo kutoka kwa taasisi za kiserikali zinazohusiana na Mamlaka Kuu ya Burudani ya Saudi Arabia, na hatimaye kusababisha kukamatwa kwake.
-
Kiongozi wa Mapinduzi atazungumza na wananchi usiku wa leo
Sambamba na Wiki Takatifu ya Ulinzi (au Wiki ya Utetezi Mtukufu - Sacred Defence), Ayatollah Khamenei atazungumza na Wananchi wa Iran na Ulimwengu mzima Usiku wa leo akidadavua masuala mbalimbali ya kitaifa na kimataifa.
-
Meja Jenerali Musawi: Jeshi la Ukombozi litatoa jibu lililo juu ya fikra za waonevu (waovu)
Rais wa Makao Makuu ya Majeshi ya Ulinzi wa Iran amesema: Tunawapa uhakika wananchi wa Iran wenye heshima na ushujaa kuwa, vikosi vya ulinzi vya Jamhuri ya Kiislamu kwa kutegemea uwezo wao, ubunifu na mshangao wa kimkakati, viko tayari kukabiliana na vitisho vyovyote vya madhalimu na waonevu wa dunia kwa majibu ya wakati muafaka, makali, ya kujutia na yaliyo zaidi ya fikra zao.
-
Mawakibu (1,800) za waombolezaji yalifurika katika Haram Tukufu ya Imam Ali (a.s) kwa Mnasaba wa kumbukumbu ya kufariki kwa Mtukufu Mtume Muhammad (s)
Haram Tukufu ya Imam Ali (a.s) Yapokea Makundi 1800 ya Waombolezaji Kutoka Ndani na Nje ya Iraq kwa Kumbukumbu ya Kifo cha Mtume Muhammad (s.a.w.w).