Rubani
-
Iran yadai kuidungua droni ya Marekani aina ya MQ-1 katika Mlango wa Hormuz
Iran imedai kuwa imeidungua droni ya kijeshi ya Marekani aina ya MQ-1 iliyokuwa ikiruka katika eneo la Mlango wa Hormuz, huku mamlaka za Marekani zikiwa hazijatoa uthibitisho wa madai hayo.
-
IRGC Yatangaza Kuiangusha Ndege ya Marekani Isiyo na Rubani Aina ya MQ-9 Kusini mwa Iran
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) limetangaza kuwa limeiangusha ndege ya Marekani isiyo na rubani aina ya MQ-9 katika anga ya mji wa Khormuj, mkoani Bushehr, kufuatia kile ilichokitaja kuwa mashambulizi ya anga ya Marekani.
-
IRGC Yatangaza Kushambulia Malengo 85 ya Kijeshi ya Marekani kwa Kujibu Mashambulizi ya Marekani
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran (IRGC) limetangaza kuwa limeanzisha hatua ya awali ya kujibu mashambulizi ya Marekani kwa kushambulia malengo 85 ya kijeshi ya Marekani katika eneo la Mashariki ya Kati kwa kutumia makombora na ndege zisizo na rubani.
-
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran: Uwezo wa Ulinzi wa Taifa Hauko Kwenye Majadiliano
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Brigedia Jenerali Ebn al-Reza, amesema uwezo wa Iran katika sekta ya ulinzi, makombora na ndege zisizo na rubani ni sehemu ya usalama wa taifa na hauwezi kujadiliwa katika mazungumzo yoyote.
-
Rubani wa Marekani Adai Kuona “Ndege zisizo na Rubani za Umbo la Jellyfish” Katika Anga ya Iran
Rubani wa ndege ya kivita aina ya F-15 ya Marekani amedai kuwa aliona kundi la ndege zisizo na rubani za Iran zikisafiri kwa mpangilio maalumu unaofanana na umbo la “jellyfish”, madai ambayo yamezua mjadala katika duru za kiintelijensia za Marekani kuhusu uwezo wa teknolojia ya droni za Iran.
-
Jeshi la Anga la Marekani Lakabiliwa na Upungufu wa Droni za MQ-9
Ripoti zimeeleza kuwa Jeshi la Anga la Marekani linakabiliwa na upungufu wa droni za MQ-9 Reaper, jambo lililoifanya Washington kutafuta njia za kuongeza idadi ya ndege hizo kwa kununua zilizopo kutoka kwa wahusika wengine.
-
Iran Yatangaza Mashambulizi ya Kulipiza Kisasi Dhidi ya Malengo ya Marekani katika Ghuba ya Uajemi
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu la Iran limesema limejibu mashambulizi ya Marekani kwa kulenga kambi za kijeshi na makao makuu ya US Fifth Fleet, huku likionya kuwa usalama wa Mlango wa Hormuz ni mstari mwekundu ambao ukiukwa utakuwa na gharama kubwa.
-
Kamati ya Uratibu ya Makundi ya Muqawama ya Iraq: Wavamizi wa Marekani Lazima Waondoke
Kamati ya Uratibu ya Makundi ya Muqawama ya Iraq imesisitiza katika taarifa yake kwamba uwepo wa majeshi ya Marekani nchini Iraq ni aina ya uvamizi unaokiuka mamlaka ya taifa hilo, na imetaka kuondoka kwa wanajeshi wa Marekani kutoka ardhi ya Iraq. “Wavamizi wanaendelea kukiuka anga la Iraq; iwe kupitia ndege zisizo na rubani (drones) au kwa kutumia ndege zao za kivita. Hatua hizi zinachukuliwa kuwa tishio kubwa kwa usalama, uthabiti na umoja wa ardhi ya nchi, na ni uvamizi wa wazi dhidi ya mamlaka na heshima ya dola ya Iraq.”
-
Ukraine Yashambulia Makaazi ya Putin kwa Ndege Droni 91 / Trump Ashtuka
Ikulu ya Kremlin jioni ya Jumatatu ilitangaza kuwepo kwa mawasiliano ya simu kati ya marais wa Urusi na Marekani, na kubainisha kuwa Rais wa Marekani, Donald Trump, alishtushwa na shambulio la ndege zisizo na rubani (droni) la Ukraine dhidi ya makaazi ya Rais wa Urusi, Vladimir Putin.
-
Je, Senario ya Maafa ya Al-Fasher Inarejelewa Tena Katika Mji wa Babanusa, Sudan?
Shirika la Umoja wa Mataifa limeonya kuwa hali ya kibinadamu katika mji wa Babanusa, uliopo katika jimbo la West Kordofan nchini Sudan, iko katika hatari kubwa ya kushuhudia janga kama lililotokea katika mji wa Al-Fasher, Kaskazini mwa Darfur, endapo hali ya sasa itaendelea kuzorota.
-