Ushujaa
-
Aida Surour:
"Kielelezo cha Ushujaa na Subira ya Mama za Mashahidi/Riwaya ya Mama wa Mashahidi Wawili wa Lebanon, Kuanzia Malezi ya Kiashura hadi Subira ya Zaynab"
Mama wa mashahidi wawili wa Lebanon, katika mahojiano na ABNA, alisimulia uzoefu wake kama mama katika njia ya muqawama na uvumilivu aliokuwa nao baada ya kuwapoteza watoto wake. Pia aliwasihi mama na wake za mashahidi waendelee kufuata njia ya wapendwa wao na kushikamana na imani.
-
Mazishi ya Mashahidi 300 Wasiojulikana Kufanyika Siku ya Kumbukumbu ya Shahada ya Bi.Fatima(sa); Dalili ya Umoja wa Kitaifa Baada ya Vita vya Siku 12
Kamanda wa Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi (IRGC) wa Mkoa Mkuu wa Tehran, Sardar Hassanzadeh, amesema kuwa miili ya mashahidi 300 wasiojulikana—ikiwa ni pamoja na 200 kwa mikoa mbalimbali na 100 kwa jiji la Tehran—iko tayari kwa ajili ya mazishi ya kitaifa. Mazishi haya yatafanyika Jumatatu tarehe 3 Azar, sambamba na kumbukumbu ya shahada ya Bibi Fatima Zahra (a.s), ambapo msafara maalumu wa “Lale za Fatima” utaanza saa 2:00 asubuhi mbele ya Chuo Kikuu cha Tehran kuelekea kwenye kituo cha "Meraje’ Shohada".
-
Pezeshkian: Jibu la ujasiri la Mwanahabari wa Kike (Simba Jike) wa Iran lilikuwa ishara ya uthabiti wa Taifa Imara la Iran
Pezeshkiani, alipongeza hatua ya mwandishi huyo wa habari wakati wa matangazo ya moja kwa moja akisema: "Maitikio ya kupongezwa ya simba jike huyu wa Iran kwenye kipindi cha moja kwa moja cha televisheni ni ishara ya upinzani (Muqawamah), uthabiti na kutoweza kushindwa kwa taifa lenye ustaarabu wa muda mrefu dhidi ya kelele za utawala usiojulikana asili yake na usio na sura halali."
-
Katika makala maalum ilijadiliwa:
Ustadi wa Kijeshi wa Waislamu wa Yemen ulivyolazimisha Marekani kufikia makubaliano? Hadithi ya Meli za Vita za Marekani - Ghuba ya Uajemi - yatoweka
Leo, Yemen imethibitisha kwa imani kwamba Marekani imepoteza heshima na hadhi yake, na imeweka mwisho kwa hadithi ya meli za kubeba ndege za kivita za Marekani ambazo zilikuwa zikiziogopesha dunia na nchi washindani wao.
-
Sababu ya Ushujaa na Ujasiri wa Ali bin Abi Talib (a.s)
Sheikh Said Othman: "Imam Ali (a.s) anakumbukwa na Ulimwengu wote wa Kiislamu kuwa yeye ni Shujaa wa Kiislamu, aliyeupigania Uislamu, na kuuhami Uislamu kwa ushujaa wake na ujasiri wake, daima aliutetea uhai wa Uislamu na aliuheshimisha Uislamu kupitia Upanga wake, kama ambavyo Ummul - Muuminina Khadija (s.a) aliuhamia na kuuheshimisha Uislamu kupitia Mali yake".
-
Imam Ali (a.s) Katika Kurasa za Historia:
Elimu na Maarifa, Ibada na Ucha Mungu, Ujasiri na Ushujaa, na Upole na Huruma ya Imam Ali (a.s)
Imam Ali (a.s) alipigwa upanga na mtu aliyejulikana kwa jina la Abdur Rahman bin Muljim Muradi (laana iwe juu yake milele). Imam Ali (a.s) alikufa Shahidi siku tatu baadaye katika usiku wa 21 wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Imam Ali bin Abi Talib (a.s) ni shakhsia wa pili mkubwa katika Uislamu baada ya Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w), na anaelezwa katika historia ya Uislamu kuwa alikuwa jasiri na shujaa wa kupigiwa mfano, mwenye imani thabiti, mwenye akhlaki njema, mwenye elimu na uadilifu usio na kifani.