Ushujaa
-
Pezeshkian: Jibu la ujasiri la Mwanahabari wa Kike (Simba Jike) wa Iran lilikuwa ishara ya uthabiti wa Taifa Imara la Iran
Pezeshkiani, alipongeza hatua ya mwandishi huyo wa habari wakati wa matangazo ya moja kwa moja akisema: "Maitikio ya kupongezwa ya simba jike huyu wa Iran kwenye kipindi cha moja kwa moja cha televisheni ni ishara ya upinzani (Muqawamah), uthabiti na kutoweza kushindwa kwa taifa lenye ustaarabu wa muda mrefu dhidi ya kelele za utawala usiojulikana asili yake na usio na sura halali."
-
Katika makala maalum ilijadiliwa:
Ustadi wa Kijeshi wa Waislamu wa Yemen ulivyolazimisha Marekani kufikia makubaliano? Hadithi ya Meli za Vita za Marekani - Ghuba ya Uajemi - yatoweka
Leo, Yemen imethibitisha kwa imani kwamba Marekani imepoteza heshima na hadhi yake, na imeweka mwisho kwa hadithi ya meli za kubeba ndege za kivita za Marekani ambazo zilikuwa zikiziogopesha dunia na nchi washindani wao.
-
Sababu ya Ushujaa na Ujasiri wa Ali bin Abi Talib (a.s)
Sheikh Said Othman: "Imam Ali (a.s) anakumbukwa na Ulimwengu wote wa Kiislamu kuwa yeye ni Shujaa wa Kiislamu, aliyeupigania Uislamu, na kuuhami Uislamu kwa ushujaa wake na ujasiri wake, daima aliutetea uhai wa Uislamu na aliuheshimisha Uislamu kupitia Upanga wake, kama ambavyo Ummul - Muuminina Khadija (s.a) aliuhamia na kuuheshimisha Uislamu kupitia Mali yake".
-
Imam Ali (a.s) Katika Kurasa za Historia:
Elimu na Maarifa, Ibada na Ucha Mungu, Ujasiri na Ushujaa, na Upole na Huruma ya Imam Ali (a.s)
Imam Ali (a.s) alipigwa upanga na mtu aliyejulikana kwa jina la Abdur Rahman bin Muljim Muradi (laana iwe juu yake milele). Imam Ali (a.s) alikufa Shahidi siku tatu baadaye katika usiku wa 21 wa Mwezi Mtukufu wa Ramadhani. Imam Ali bin Abi Talib (a.s) ni shakhsia wa pili mkubwa katika Uislamu baada ya Mtukufu Mtume Muhammad (s.a.w.w), na anaelezwa katika historia ya Uislamu kuwa alikuwa jasiri na shujaa wa kupigiwa mfano, mwenye imani thabiti, mwenye akhlaki njema, mwenye elimu na uadilifu usio na kifani.