ibada
-
Zaidi ya Mahujaji 5,000 wa Umrah Wamewasili Nchini Saudi Arabia
Shirika la Hija na Ziara nchini Iran limetangaza kuwa idadi ya mahujaji wa Umrah waliopelekwa katika ardhi takatifu tangu kuanza kwa msimu wa Umrah wa mwaka 1445 Hijria (sawa na 1404 kwa kalenda ya Iran), kuanzia tarehe 1 Shahrivar, imefikia zaidi ya watu 5,000.
-
Ayatollah Makarim Shirazi: Baraza la Uratibu wa Matangazo Lina Nafasi Muhimu Katika Kulinda Mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu
Ayatollah Makarim Shirazi amethibitisha kwamba Baraza la Uratibu wa Matangazo ya Kiislamu lina mchango mkubwa usio na mfano katika kuhifadhi mfumo wa Jamhuri ya Kiislamu.
-
Imam Khomeini (r.a) – Ni Kiongozi wa Kidini au wa Kitaifa
Imam ni sehemu ya utambulisho wa kitaifa na miongoni mwa fahari za nchi yetu, na ana sifa na tofauti na viongozi wengine wa kitaifa ambazo zinaonyesha ubora wake juu ya wengine.
-
Kiongozi wa Mapinduzi: "Hakuna manufaa yoyote kwa Umma wa Kiislamu yaliyo juu ya Umoja"
Kiongozi Muadham wa Mapinduzi ameeleza katika Mkutano na wahusika wa Hajj na baadhi ya Waumini waliotembelea Nyumba Tukufu (Al-Kaaba) kwamba: "Muundo na sura ya nje ya ibada hii ni ya kisiasa kabisa, lakini maudhui ya vipengele vyake ni ya kiroho na ya ibada, ili manufaa ya Wanadamu wote yaweze kutimizwa. Na leo, faida kubwa kwa Umma wa Kiislamu ni 'Umoja na Ushirikiano' ili kutatua matatizo ya Ulimwengu wa Kiislamu. Ikiwa umoja huu ungelikuwepo, matatizo kama ya Gaza na Yemen yasingekuwepo."
-
Ibada za kufanya Usiku wa 23 wa Lailatul-Qadri
Inapendekezwa kusoma Dua ya (......يا مُدَبِّرَ الاُمُورِ ) hali ya kuwa umerukuu, umesujudu, umesimama, umekaa na irudierudie kila sehemu, na isome hata kila siku na iombe Dua hii kwa wingi katika Usiku wa mwisho wa Ramadhani Tukufu.
-
Fadhila za Mwezi Mtukufu wa Ramadhan:
Tusiwe wavivu ndani ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, na tusichoke kuomba Maghfira na Msamaha
Kila kizuri unachokifanya ndani ya Mwezi Mtukufu wa Ramadhan, ni thawabu.Hata pumzi zetu tunapopumua ndani ya Mwezi huu, hilo linahesabiwa kuwa ni ibada, na hata kulala kwetu na usingizi wetu ndani yake pia ni ibada. Sisi ni wageni wa Mwenyezi Mungu ndani yake.