kikanda
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Ugiriki wafanya mazungumzo ya simu kuhusu masuala ya kimataifa na kikanda
Abbas Araghchi na George Gerapetritis wamejadili masuala ya uhusiano wa nchi mbili pamoja na maendeleo ya hivi karibuni ya kimataifa na kikanda.
-
Pakistan: Ziara ya Waziri wa Mambo ya Ndani Tehran Kulenga Kuimarisha Amani na Usalama wa Kikanda
Pakistan imesema ziara ya Waziri wa Mambo ya Ndani, Mohsin Naqvi, nchini Iran inalenga kuendeleza mashauriano na Tehran kuhusu kuimarisha uhusiano wa pande mbili, ushirikiano wa kiusalama na juhudi za kuimarisha amani na utulivu katika eneo.
-
Araghchi Azungumza na Mawaziri wa Saudi Arabia na Pakistan Kuhusu Kuimarisha Usalama wa Asia Magharibi
Iran, Saudi Arabia na Pakistan zimesisitiza umuhimu wa kuimarisha ushirikiano wa kikanda na kutumia njia za kidiplomasia pamoja na suluhu za kisiasa ili kudumisha usalama na utulivu katika eneo la Asia Magharibi.
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na India wazungumza kwa simu kuhusu uhusiano wa pande mbili na hali ya kikanda
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Abbas Araghchi, na mwenzake wa India, Subrahmanyam Jaishankar, wamefanya mazungumzo ya simu yaliyojikita katika kuimarisha ushirikiano wa nchi zao pamoja na kujadili maendeleo ya hivi karibuni katika eneo na duniani.
-
Waziri Mkuu wa Iraq Aagiza Kuimarishwa kwa Tahadhari na Ulinzi wa Kijeshi Nchini Kote
Msemaji wa Amiri Jeshi Mkuu wa Iraq amesema Waziri Mkuu ameagiza kuongezwa kwa kiwango cha tahadhari na utayari katika kambi na vituo vyote vya kijeshi, pamoja na kuharakisha uimarishaji wa mifumo ya rada, ulinzi wa anga na mipango ya kiintelijensia ili kuzuia vitisho vyovyote vya kiusalama.
-
Pakistan Yaonya Iran: Mashambulizi Dhidi ya Saudi Arabia ni “Mstari Mwekundu”
Pakistan imewasilisha ujumbe kwa Iran kwamba mashambulizi dhidi ya Saudi Arabia, yakiwemo mashambulizi yanayofanywa na harakati ya Ansarullah ya Yemen, yatachukuliwa kuwa mashambulizi dhidi ya Pakistan. Onyo hilo linakuja huku Islamabad ikihofia kuvutwa katika mzozo mpana kati ya Marekani, Iran na washirika wao wa kikanda.
-
Iran Yalaani Vikali Shambulio la Kigaidi Kusini Magharibi mwa Pakistan
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran, Ismail Baqaei, amelaani vikali shambulio la kigaidi lililotokea katika mji wa Khuzdar kusini magharibi mwa Pakistan, akitoa salamu za pole kwa familia za wahanga na kusisitiza umuhimu wa ushirikiano wa kikanda katika kupambana na ugaidi.
-
Umoja wa Ulaya Washindwa Kufikia Makubaliano Kuhusu Kumuwekea Vikwazo Itamar Ben-Gvir
Msemaji wa masuala ya nje wa Tume ya Ulaya amesema kuwa nchi wanachama wa Umoja wa Ulaya hazikufikia mwafaka kuhusu pendekezo la kumuwekea vikwazo Waziri wa Usalama wa Ndani wa Israel, Itamar Ben-Gvir, huku zikilaani kauli zake za uchochezi dhidi ya Lebanon.
-
Rais wa Iran Aishukuru Qatar kwa Jukumu Lake la Kupunguza Mvutano na Kuendeleza Diplomasia
Rais wa Iran, Masoud Pezeshkian, ameipongeza Qatar kwa mchango wake katika kupunguza mvutano wa kikanda na kuwezesha juhudi za kidiplomasia zilizopelekea kufikiwa kwa makubaliano ya kumaliza vita.
-
Abdul-Malik al-Houthi: Yemen Iko Tayari kwa Hatua Yoyote ya Kuongezeka kwa Mzozo
Kiongozi wa harakati ya Ansarullah ya Yemen, Abdul-Malik al-Houthi, amesema kundi hilo liko tayari kwa hatua yoyote ya kuongezeka kwa mzozo katika Mashariki ya Kati, huku akisisitiza kuwa linaendelea kuratibu kwa karibu na washirika wake wa Muqawama kuhusu maendeleo ya Lebanon na Palestina.
-
Kamanda Iran: Tulishambulia Kambi 17 za Marekani na Kufanya Zaidi ya Operesheni 100 Kijeshi
Kamanda wa Ulinzi wa Anga wa Jeshi la Iran kaskazini mwa nchi amedai kuwa Iran ililenga kambi 17 za kijeshi za Marekani katika eneo la kikanda na kufanya zaidi ya operesheni 100 za kijeshi zilizofanikiwa, akisisitiza kuwa mashambulizi hayo yalikuwa sehemu ya “vita vya kikanda” na kwamba mipango ya Marekani na Israel ya kuidhoofisha Iran ilishindwa.
-
Iraq yakataa kuruhusu matumizi ya anga lake kwa mashambulizi dhidi ya Iran
Tamko la Iraq linaonyesha kuwa Iraq inalinda mamlaka yake na haitaki kuhusishwa na migogoro ya kijeshi katika eneo hilo, ikisisitiza sera ya kudumisha usalama na utulivu wa kikanda.
-
Reuters: Iran Yasisitiza Haki ya Kurutubisha Uranium Katika Mazungumzo ya Muscat
Reuters yaripoti kuwa Iran imesisitiza haki yake ya kurutubisha uranium katika mazungumzo ya Muscat, huku ikionyesha utayari wa kujadiliana kuhusu kiwango cha urutubishaji au kuanzishwa kwa consortium ya kikanda, na ikaongeza kuwa masuala ya makombora hayakujumuishwa kwenye ajenda ya mazungumzo.
-
Hadhramaut; Moyo wa Mafuta wa Yemen na Kitovu cha Ushindani kati ya Saudi Arabia na Falme za Kiarabu (UAE)
Mkoa wa Hadhramaut, eneo kubwa zaidi na lenye utajiri mkubwa wa mafuta nchini Yemen, kwa sasa umegeuka kuwa kitovu cha ushindani kati ya Saudi Arabia na Falme za Kiarabu. Licha ya vita vilivyoendelea kwa zaidi ya muongo mmoja, Hadhramaut kwa kiasi kikubwa imeepuka mapigano ya moja kwa moja kati ya serikali ya Yemen iliyojiuzulu na serikali inayoungwa mkono na Harakati ya Ansarullah; hata hivyo, mkoa huu haujaepuka athari za vita na mashindano ya ushawishi wa ndani na kikanda.
-
Waziri Mkuu wa utawala wa Kizayuni wa Israel anatarajiwa katika kikao chake na Rais wa Marekani
Kuwasilisha chaguo mbalimbali za mashambulizi mapya yanayoweza kufanywa na Israel dhidi ya Iran, pamoja na kujadiliana kuhusu hali tofauti za kijeshi na athari zake kwa usalama wa kikanda.
-
Iran: Kukabiliana na ugaidi kunahitaji ushirikiano wa kikanda, hasa na Afghanistan
Katibu wa Baraza Kuu la Usalama wa Taifa la Iran alitangaza kuwa makundi ya kigaidi hayapo tu nchini Afghanistan, bali yameenea katika nchi mbalimbali za eneo hilo. Alisisitiza kuwa kukabiliana na tishio hili kunahitaji ushirikiano wa pamoja wa nchi jirani, hasa Afghanistan.
-
Ayatollah Khamenei Asifu Uwezo wa Makombora ya Iran, Asema Yameharibu Vituo Muhimu vya Utawala wa Kizayuni
Ayatollah Khamenei pia aliongeza kuwa utawala wa Kizayuni (Israel), ambao kwa muda mrefu umekuwa ukifanya vitisho na mashambulizi dhidi ya eneo hili la kikanda, sasa “umepokea funzo ambalo litabaki kwenye kumbukumbu zake,” akisisitiza kuwa taifa la Iran halitasita kujibu hatua yoyote ya uchokozi
-
Doha kuandaa mkutano wa dharura wa Kiarabu-Kiislami baada ya shambulio la Israel
Ijumaa, Qatar ilikaribisha hatua ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kulaani shambulio la Israel dhidi ya ujumbe wa Hamas mjini Doha, ikilitaja shambulio hilo kama “la usaliti” na ukiukaji wa kanuni za kimataifa.