Rais wa Majlisi ya Ushauri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Bagher Ghalibaf, amesisitiza umuhimu wa kuimarisha uhusiano wa kimkakati, kisiasa na kibunge kati ya Iran na China, akibainisha kuwa mabadiliko ya hivi karibuni ya kikanda na kimataifa yameufanya ushirikiano wa karibu kati ya Tehran na Beijing kuwa wa lazima zaidi kuliko wakati wowote.
Wakati ambapo Waislamu wa Kisunni wameshindwa kufikia mwafaka juu ya mgombea mmoja, hatima ya urais wa Bunge la Iraq imefungamana zaidi kuliko wakati mwingine wowote na maamuzi pamoja na hesabu za kisiasa za Waislamu wa Kishia na vyama vya Kikurdi.