Maafisa wa Seminari (Hawzat) hii walisema kwamba lengo la kufanya mashindano haya lilikuwa ni kukuza elimu ya Ahlul-Bayt (a.s) na kuwafahamisha wanafunzi mawazo yenye nuru ya Amirul-Mu'minina (a.s) na kuimarisha moyo wa utafiti na udadisi.
Wanafunzi wa Kike na Kiume wa Shule ya "Wilayat" ya Bamyan, huku wakisoma kwa makini Barua ya 31 ya Nahj al-Balagha, ambayo ina ushauri wa kibaba wa Amirul Muminina (a.s) kwa Mtoto wake Imam Hassan (a.s), na inayojulikana zaidi kama moja ya vyanzo vya Kimaadili na Kimalezi, walishiriki katika shindano hilo la Kisayansi na kiroho.
