14 Januari 2025 - 21:05
Kundi la Wayahudi liliziomba nchi zote za dunia kukata uhusiano wao na Israel

Likisisitiza kuwa Israel iliasisiwa juu ya "itikadi mbovu" ya Uzayuni, kundi la Kiyahudi la "Yehudit Torah" lilizitaka nchi zote za dunia kukata uhusiano wao na utawala huo.

Kundi hili la Kiyahudi liliandika katika ujumbe wa X: Tunaziomba nchi na mataifa yote kukata uhusiano wote na Israel na Wazayuni, tusiwasaidie na tusiwaruhusu kuingia katika nchi yao, kwa sababu ikiwa watahisi kuwa wewe ni dhaifu walau kidogo, watajaribu kukuponda, kukutawala na kukufanya mtumwa wao.

Kundi hili liliwasilisha Uzayuni kuwa itikadi potovu iliyoanzishwa na mtu asiyeamini kuwa kuna Mungu aitwaye Theodor Hertzel.

Kundi hili liliendelea: Uzayuni hauna uhusiano wowote na Wayahudi na Uyahudi; Lengo la Wazayuni ni kuugeuza Uzayuni kuwa Dini ya Mayahudi na kuuangamiza Uyahudi.