Ayatollah Sayyid Mojtaba Khamenei
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah na Mashahidi Wenzake Waliugeuza Mche wa Muqawama Kuwa Mti Imara
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba Khamenei, amesema Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah na mashahidi wenzake waliugeuza mche wa Muqawama wa Kiislamu kuwa mti mkubwa na imara ulioipa Lebanon heshima na utukufu katika Ulimwengu wa Kiislamu.
-
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu: Mazishi ya Mamilioni ya “Mbeba Bendera wa Muqawama” Nchini Iraq Yamebadilisha Mizani ya Madola ya Kiburi
Kiongozi Mkuu wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, amewapongeza wananchi wa Iraq kwa kuandaa mazishi makubwa na ya kihistoria ya kiongozi shahidi wa Muqawama, akisisitiza kuwa ushiriki wa mamilioni ya wananchi wa Iran na Iraq umeonesha mshikamano wa kina na undugu wa mataifa hayo mawili na kuvuruga njama za maadui za kuleta mgawanyiko.
-
Ayatullah Mujtaba al-Husseini Khamenei: Shahidi Aliishi na Kupigania Njia ya Imam Hussein (AS)
Ayatullah Sayyid Mujtaba al-Husseini Khamenei amesema kuwa kiongozi shahidi aliishi, akafikiri, akapambana na hatimaye akapata shahada kwa kufuata kwa dhati njia na mafundisho ya Imam Hussein (AS).
-
Kiongozi wa Mapinduzi: Kulipiza kisasi hakutategemea uwepo wangu au wa viongozi wengine
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema kuwa kuwawajibisha waliohusika na mauaji ya Kiongozi Shahidi ni jambo ambalo litaendelea bila kutegemea uwepo wake binafsi au wa viongozi wengine, akisisitiza kuwa watu huru duniani watatekeleza wajibu wao kwa wakati wake.
-
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba al-Husseini Khamenei, Atoa Tamko Maalumu Kufuatia Mazishi ya Imam Shahidi Sayyid Ali Khame
Katika tamko lake kufuatia mazishi makubwa ya Imam Shahidi Sayyid Ali Khamenei, Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatullah Sayyid Mujtaba al-Husseini Khamenei, amesisitiza kuendelezwa kwa njia ya Imam Husayn (a.s.), kulinda urithi wa Mapinduzi ya Kiislamu, na kuendelea kudai haki kwa damu za mashahidi.
-
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran: Tumeanza Enzi Mpya Chini ya Uongozi wa Ayatollah Sayyid Mojtaba Khamenei
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran, Mohammad Reza Aref, amesema Jamhuri ya Kiislamu imeanza enzi mpya chini ya uongozi wa Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, akitoa shukrani kwa mahudhurio makubwa ya wananchi wa Iran na Umma wa Kiislamu katika mazishi ya Kiongozi Shahidi.