Kwa Mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (a.s) –ABNA– Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu, Ayatollah Sayyid Mujtaba Khamenei, ametoa salamu na heshima kwa roho ya Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah, viongozi waliotangulia wa Muqawama wa Kiislamu na mashahidi wote waliokuwa pamoja naye, akisema waligeuza mche wa Muqawama wa Kiislamu kuwa mti mkubwa na imara wenye mizizi thabiti na matawi yaliyonyanyuka juu.
Katika ujumbe wake wa kujibu barua ya kuahidi utii (bay'ah) iliyotumwa na wapiganaji waaminifu na mashujaa wa Hizbullah ya Lebanon, Kiongozi huyo alinukuu aya ya Qur'ani Tukufu: "Asili yake ni thabiti na matawi yake yako mbinguni", akieleza kuwa Muqawama umejengwa juu ya misingi madhubuti ya imani, kujitolea na kujitolea muhanga kwa ajili ya kulinda heshima ya Umma wa Kiislamu.
Ayatollah Khamenei alisisitiza kuwa juhudi na mapambano ya Shahidi Sayyid Hassan Nasrallah pamoja na wenzake yaliipa Lebanon heshima, nguvu na hadhi kubwa katika Ulimwengu wa Kiislamu, na kwamba mchango wao utaendelea kuwa chanzo cha msukumo kwa vizazi vijavyo vya wapigania haki na uhuru.

Maoni yako