10 Julai 2026 - 17:45
Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran: Tumeanza Enzi Mpya Chini ya Uongozi wa Ayatollah Sayyid Mojtaba Khamenei

Makamu wa Kwanza wa Rais wa Iran, Mohammad Reza Aref, amesema Jamhuri ya Kiislamu imeanza enzi mpya chini ya uongozi wa Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, akitoa shukrani kwa mahudhurio makubwa ya wananchi wa Iran na Umma wa Kiislamu katika mazishi ya Kiongozi Shahidi.

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) –ABNA– Makamu wa Kwanza wa Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Mohammad Reza Aref, amepongeza mahudhurio makubwa na ya kihistoria ya wananchi wa Iran pamoja na Umma wa Kiislamu katika shughuli za kumuaga na kumzika Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu.

Katika ujumbe alioutuma kwa wananchi wa Iran, Aref alisema kuwa Jamhuri ya Kiislamu imeanza enzi mpya chini ya uongozi wa Ayatullah Sayyid Mojtaba Khamenei, mtoto wa Kiongozi Shahidi, akisisitiza kuwa taifa litaendelea kusonga mbele kwa mshikamano wa kitaifa, ari ya kujitolea na juhudi maradufu.

Aref alieleza kuwa historia ya kila taifa huwa na nyakati ambazo uimara wake hupimwa katikati ya majonzi makubwa, na kwamba mahudhurio ya kipekee ya wananchi katika ibada za kuaga zilizofanyika kwa siku mbili mjini Tehran, mazishi yaliyofanyika Tehran na Qom, pamoja na upyaisho wa ahadi uliofanyika Najaf na Karbala, ni ushahidi wa uaminifu na mshikamano wa Umma wa Kiislamu.

Aidha, alisema kuwa mazishi na kuzikwa kwa Kiongozi Shahidi karibu na haram ya Imam Ali ibn Musa al-Ridha (as) katika mji wa Mashhad kumehitimisha tukio la kihistoria lililoonyesha kwa vitendo mapenzi, utii na mshikamano wa wananchi wa Iran na Waislamu kwa ujumla.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha