Fadhila
-
Usijivune kwa Maneno Maneno na Kujiona Mwenye Fadhila | Ibada na Jema lolote bila Unyenyekevu, ni Njia ya kupoteza kila Kheri
Baadhi ya Mabedui walikuwa wakimfanyia Mtume (s.a.w.a) madai ya fadhila kwa kusilimu kwao, kama Qur’ani inavyosema: “Wanakuonea fadhila kwa kusilimu kwao.” Basi Qur’ani ikawafunza adabu kwa kusema: “Sema: Msinionee fadhila kwa Uislamu wenu; bali Allah ndiye anayekuoneeni fadhila kwa kuwaongoza kwenye imani, ikiwa nyinyi ni wakweli.” (Al-Hujurāt: 17).
-
Mkutano wa Tatu wa Kitaaluma kuhusu Maombolezo na Desturi za Kidini; Kusisitiza nafasi ya kihadhari ya Hay’a katika jamii na familia
Hujjatul-Islam wal-Muslimin Babakhani pia alisisitiza nafasi ya wanawake katika hay’a na kusema: “Tangu kuundwa kwa hay’a, wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika uongozi wa kitamaduni na kidini - kuanzia Bibi Fatima az-Zahra (a.s) na Bibi Zaynab (a.s) hadi leo - na wametoa mchango mkubwa katika kuhifadhi na kueneza utamaduni wa hay’a. Uwepo wao umeleta athari kubwa katika kufundisha mafundisho ya dini na kuonyesha kwa jamii fadhila za Ahlul-Bayt (a.s).”
-
Darsa Fupi na Muhimu Katika Muktadha wa Maombolezo ya Bibi Fatimah az-Zahra (a.s) kuhusu "Fadhila na Siri za Tasbihat az-Zahra (a.s) na Ayatul Kursi"
Imam al-Baqir (a.s.) amesema: “Anayesema Tasbih ya Fatimah az-Zahra (a.s.) kisha akaomba maghfirah, atasamehewa. (Tasbih hiyo inaposomwa na mja) Ni mia moja kwa ulimi wake, lakini ni elfu moja katika mizani.”
-
Dalili ya wazi na kubwa Kuhusu Kupigana kwa Malaika Pembeni ya Ali (as)
kwa Hakika Amirul-Mu'minin Ali (a.s) hakuwa anarudi kutoka vitani mpaka apate ushindi kwa msaada wa Mwenyezi Mungu. Na ni fadhila iliyo kubwa kiasi gani kuwa Malaika Jibril (as) anapigana upande wa kulia wake, na Mikail (as) upande wa kushoto wake.