Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Brigedia Jenerali Ebn al-Reza, amesema uwezo wa Iran katika sekta ya ulinzi, makombora na ndege zisizo na rubani ni sehemu ya usalama wa taifa na hauwezi kujadiliwa katika mazungumzo yoyote.
Kaimu Waziri wa Ulinzi wa Iran amesema kuwa wananchi wa Iran, kwa uungwaji mkono wa vikosi vya jeshi, wamefanikiwa kuwalazimisha maadui kupata “ushindi wa kihistoria”, akisisitiza pia umuhimu wa kuimarisha umoja wa Waislamu kupitia Eid al-Adha na msimu wa Hija.