"Vikwazo na orodha ya ugadi ni mbinu mpya ya kulishambulia kundi letu na lazima tukabiliane nao kwa kadri ya uwezo” alisema kupitia hotuba ya televisheni, akitoa wito kwa wafuasi wao kuliunga mkono kundi hilo kwa kutoa mchango.
Uwezo wa nguvu za kijeshi wa Hezbollah na umiliki wa aina mbalimbali ya makombora unaipa wasiwasi Israel ambayo imedhulumu ardhi za waarabu ikiwemo Lebanon.
Israel ambayo ilijigamba kwa nguvu na uwezo wake wakijeshi kwasasa imejikuta ikijijengea kuta na mahandaki ili kujihifadhi na mashambulizi ya kundi dogo tu la wapiganaji wa Hibullah.