Lugha
-
Jukumu la Marajii wa Kidini wa Kishia katika;
"Kulinda Umoja wa Kitaifa na Utambulisho wa Iran / Sehemu ya Saba: Kisa cha Kuokolewa kwa Lugha ya Taifa ya Iran na Ukombozi wa Azarbaijan"
Kulinda umoja wa ardhi na kuzingatia utambulisho wa kidini ni miongoni mwa masuala yaliyokuwa yakipewa umuhimu mkubwa na viongozi wa kidini katika ardhi za Kiislamu. Kiasi kwamba kila aina ya uvamizi au shambulio dhidi ya ardhi za Kiislamu ilikabiliwa na mwitikio mkali kutoka kwao. Uvamiuzi wa Azarbaijan wakati wa Vita vya Pili vya Dunia na juhudi za kuutenga mkoa huo kutoka Iran ni miongoni mwa mambo yaliyodhihirisha tena ushawishi wa uongozi wa kidini katika kulinda umoja wa ardhi ya nchi. Aidha, kulinda utambulisho wa kitaifa wa Kiairani pia lilikuwa ni mojawapo ya masuala yaliyopatiwa umuhimu maalum na viongozi (Marajii) wa kidini katika kipindi cha utawala wa Pahlavi.
-
Sisi na wamagharibi kwa Mtazamo wa Imam Khamenei – Mkutano Uliofanyika Nchini Kenya +Picha
Pourmarjan: “Ayatollah Khamenei, kama mwanafiqhi na mwanafikra mashuhuri katika ulimwengu wa Kiislamu, na ambaye ametumia zaidi ya miaka sitini katika nyanja za kielimu, kidini, kitamaduni, na kisiasa, ametoa mitazamo sahihi na ya kimkakati kuhusu Magharibi. Uelewa wa fikra hizi ni muhimu sana kwa kizazi cha leo cha vijana na wasomi.”
-
"Ayatollah Ramezani: Chuo cha Dini cha Qom kina uwezo wa kuunda ustaarabu wa Kiislamu / Mapinduzi ya Kiislamu yamebadilisha mlingano wa dunia."
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul-Bayt (a.s) alisema: Leo hii, fursa ya kipekee imepatikana kwa vyuo vya kidini, ambayo haijawahi kushuhudiwa katika vipindi vya nyuma. Tunapaswa kuweza kuitambulisha dini ya Uislamu kwa dunia kwa kutumia lugha na istilahi za kimataifa, na kwa hakika tutafaulu katika njia hii.
-
Mwenyekiti wa Bunge la Umoja wa Waislamu wa Pakistan:
Kila siku huko Gaza ni Apocalypse (Zama za Mwisho / Mwsiho wa Dunia) / Ukimya wa watawala wa Kiarabu unatia uchungu zaidi kuliko uhalifu (jinai)
Mwenyekiti wa Baraza la Umoja wa Waislamu wa Pakistan amesema: "Tukio chungu zaidi si tukio la uhalifu unaofanyika dhidi ya Gaza, bali ni kile kimya kinachojiri katika Kasri za watawala wa Kiislamu na Kiarabu." Lugha zilizokuwa zikizungumza kutetea Uislamu sasa hivi zinalamba nyayo za madola ya kibeberu.