Mkubwa
-
Wizara ya Usalama ya Iran Yapongeza Mahudhurio Makubwa ya Umma wa Kiislamu Katika Mazishi ya Kiongozi Shahidi
Wizara ya Usalama ya Jamhuri ya Kiislamu ya Iran imetoa taarifa ya kupongeza ushiriki mkubwa wa wananchi, Marjaa wa dini, serikali na wajumbe kutoka nchi mbalimbali za Kiislamu katika mazishi ya Kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu, ikieleza kuwa tukio hilo limeonyesha umoja, uaminifu na mshikamano wa Umma wa Kiislamu.
-
Lariijani: Ushiriki Katika Mazishi ya Shahidi Ni Ishara ya Imani, Utii na Azma ya Taifa
Mwenyekiti wa Baraza la Uamuzi wa Maslahi ya Mfumo wa Kiislamu ameueleza kuwa kushiriki katika hafla ya kuaga kiongozi Shahidi wa Mapinduzi ya Kiislamu ni ishara ya imani, utii na azma ya umma uliosimama katika njia ya uhuru, heshima na muqawama.
-
Siku Tano Zasalia kwa Kuaga Mwili wa Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Shahidi, Imam Sayyid Ali Khamenei
Kamati ya maandalizi ya mazishi ya Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu Shahidi, Imam Sayyid Ali Khamenei (q.s), imetangaza kuwa zimebaki siku tano pekee kabla ya kufanyika kwa hafla ya mwisho ya kuuaga mwili wa kiongozi huyo, aliyesimama kidete kupinga mfumo wa dhulma wa kikanda kwa msaada wa Muqawama.
-
Maqamu ya Tall al-Zaynabiyyah katika Karbala Tukufu Yafunguliwa Rasmi Baada ya Miaka ya Ujenzi
Baada ya miaka kadhaa ya ujenzi na ukarabati, Maqam ya Tall al-Zaynabiyyah katika mji mtukufu wa Karbala imefunguliwa rasmi, na waumini wengi wamepokea kwa furaha kufunguliwa kwa eneo hili lenye umuhimu mkubwa katika historia ya tukio la Ashura.
-
Jenerali Ismail Qa'ani: Gaza pia ina “Tufani” yake; msidharau uwezo wa Muqawama
Kamanda wa Kikosi cha Quds katika Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC), Jenerali Ismail Qa'ani, ameonya kuwa Gaza pia ina uwezo mkubwa wa kujibu mashambulizi, akisema kuwa kupuuza maonyo ya Muqawama kunaweza kusababisha hasara kubwa zaidi.
-
Mjadala Mkubwa Wazuka Mitandaoni Kuhusu Taarifa Zinazokinzana za Uwezo wa Kijeshi wa Iran
Watumiaji wa mitandao ya kijamii wamehoji taarifa zinazokinzana kuhusu uwezo wa kijeshi wa Iran, baada ya baadhi ya vyombo vya habari kudai kuwa umedhoofika pakubwa huku matukio ya baadaye yakionyesha Iran ikiendelea na operesheni za kijeshi, hali iliyozua mjadala kuhusu ukweli wa taarifa hizo.
-
Ripoti ya The New York Times kuhusu kesi ya Jeffrey Epstein: Mtandao wa ushawishi bila uwajibikaji
Ripoti ya gazeti la The New York Times inafichua jinsi Jeffrey Epstein alivyokuwa na mtandao mkubwa wa wanasiasa, wafanyabiashara, na watu mashuhuri waliokuwa wakiufaidi ushawishi wake bila uwajibikaji. Licha ya ufichuzi huu mkubwa, hakuna mmoja kati ya watu hawa aliyehukumiwa, jambo linaloongeza kutoaminiana kwa umma na kuibua uvumi kuhusu vifo vya Epstein gerezani mwaka 2019.
-
Tarehe 13 Rajab: Maadhimisho ya Kuzaliwa kwa Kiongozi Mkuu wa Umma, Imam Ali (a.s)
Tarehe 13 ya mwezi wa Rajab ni siku ya kuzaliwa kwa Imam Ali (a.s), kiongozi mkuu baada ya Mtume Muhammad (s.a.w.w), ambaye ni mtu pekee aliyezaliwa ndani ya Al-Kaaba Tukufu na anayetambuliwa kwa elimu, uadilifu, ujasiri na maadili mema kwa wanadamu wote.
-
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Iran Lafichua Droni Mpya ya Kujitoa Mhanga ya Kasi ya Juu imayoitwa: “Hadid-110 | Hadid yaani: Chuma
Hadid-110 ilizinduliwa kwa kutumia mfumo wa reli unaosaidiwa na roketi, hali inayoiwezesha kufikia kasi ya juu mara baada ya kurushwa. Muundo wake wa kisasa unaojumuisha injini ndogo ya jet na umbo lenye pembe maalumu (low-observable faceted design) umeundwa mahsusi ili kupunguza uwezekano wa kugunduliwa na mifumo ya ulinzi wa anga.
-
Kuomba Mvua katika Fikra za Kiislamu na Kishia / Sehemu ya Kumi; Nafasi ya Uimamu katika Kushuka kwa Mvua ya Rehema
Sala ya kuomba mvua ya Imam Reza (a.s) ni miongoni mwa matukio maarufu ya kihistoria ambayo ndani yake, mbali na kusisitiza juu ya kuomba na kumlilia Mwenyezi Mungu, pia imebainishwa nafasi maalumu ya Uimamu na Ahlul-Bayt (a.s) katika kushuka kwa mvua ya rehema ya Mwenyezi Mungu.
-
Mchambuzi wa Zamani wa CIA: Uwezo wa Kijeshi wa Iran Sasa Ni Imara Zaidi na Marekani Haiwezi Kamwe Kuilazimisha Iran Ijisalimishe
Johnson anaamini kuwa Iran sasa si tu haiko dhaifu, bali imejizatiti kama mchezaji mkuu katika masuala ya kieneo, na ina uwezo wa kushughulikia changamoto na shinikizo kutoka nje.
-
Hadhramout Yadhibitiwa na Baraza la Mpito la Kusini: Ramani Mpya ya Madaraka Mashariki mwa Yemen
Hadhramout, jimbo kubwa na lenye utajiri mkubwa zaidi nchini Yemen, limeingia rasmi kwenye udhibiti wa Baraza la Mpito la Kusini (STC) baada ya kusonga mbele kwa kasi kwa vikosi vyake. Hatua hii imeufanya mkoa huo kuwa uwanja muhimu wa kuchorwa upya kwa ramani ya madaraka mashariki mwa Yemen.
-
Sheikh Naim Qassem:
Lebanon inapaswa kukabiliana kikamilifu na uvamizi wa kibeberu wa utawala wa Kizayuni | Mashahidi walijitolea kwa roho, mali na kila walichokuwa nacho
Lebanon inakabiliwa na uvamizi hatari wa Kizayuni: Akirejea mashambulizi ya mara kwa mara ya Israel kusini mwa Lebanon, alisema: “Lebanon inakabiliwa na uvamizi wa hatari na wa kupanua mipaka wa utawala wa Kizayuni. Lazima tukabiliane nao kwa kila njia na mbinu. Adui huyu haheshimu makubaliano yoyote.”
-
Mkataba wa mabilioni kadhaa ya dola wa Israel kwa ajili ya kuongeza uzalishaji wa ngao ya Chuma (Iron Dome)
Wizara ya Ulinzi ya Israel imetiliana saini mkataba mkubwa na Kampuni ya Rafael ili kuongeza kwa kiasi kikubwa uzalishaji wa makombora ya kukinga ya mfumo wa Iron Dome (Gombo la Chuma).
-
Shukrani za Ayatollah Nouri Hamadani kwa jitihada za Ofisi ya Vikundi vya Misikiti katika shughuli za Qur’an / Ihitaji uwepo mkubwa zaidi wa vijana katika Misikiti.
Kiongozi wa kiitikadi wa Mashia alisema kuwa: ‘Msikiti usio na vijana hauwezi kustawi, na uwepo wa vijana katika misikiti ni wa thamani sana.’ Alisisitiza: ‘Ninashukuru na kupongeza jitihada za Vikundi vya Utamaduni na Sanaa vya Misikiti katika shughuli za Qur’an na uhai wa misikiti, na nina matumaini uwepo wa vijana katika misikiti utakuwa mkubwa zaidi.
-
Usafishaji Mkubwa wa Maficho ya ISIS katika Mikoa 4 ya Iraq
Kwa kushirikiana na Idara ya Kitaifa ya Ujasusi ya Iraq, maficho 10 na mitaro 3 imepekuliwa katika Kirkuk, huku pango moja la mawe katika mkoa wa Diyala likiharibiwa.