Huku Ghaza ikipamba moto kutokana na uvamizi wa utawala ghasibu wa Kizayuni, wanazuoni wa Bahrain kwa kauli iliyo wazi wamepongeza kusimama kidete wananchi wa Palestina na kulaani mauaji ya kudumu na kimya cha kutisha cha taasisi za kimataifa na nchi za Kiarabu.
Umoja wa Wanazuoni wa Kiislamu Ulimwenguni umetoa Fat'wa kuhusu Wajibu wa Jihadi katika kuunga mkono Ghaza na kusisitiza kuwa, Jihadi dhidi ya utawala wa Kizayuni na mamluki na askari wake wanaohusika na mauaji ya halaiki ya watu wa Ghaza katika ardhi zinazokaliwa kwa mabavu za Palestina ni wajibu mutlaki (unaomgusa kila mtu).