Ofisi
-
Naibu wa Ofisi ya Tablighi ya Hawza ya Qom amesema kuwa:
“Utetezi Mtakatifu (Kujihami Kutakatifu - Sacred Defence) ni chuo cha malezi na hazina ya kitamaduni”
Hujjatul-Islam Rousta Azad amesema: Kongamano la “Muballighina Mujahid” likiambatana na kumbukumbu ya kuwatunukia mfano bora wa jihadi na tabligh, litafanyika siku ya Jumatano, tarehe 9 Mehr, kuanzia saa 3 asubuhi, kwa kuhudhuriwa na kundi muhimu la makamanda na mashahidi hai wa Vita vya Utetezi Mtakatifu, katika ukumbi wa kimataifa wa mikutano wa Ghadir, Ofisi ya Tablighi ya Kiislamu.
-
Malta Yaitambua Rasmi Palestina
Malta imetangaza kuwa leo itaikubali rasmi Palestina kama taifa huru.
-
Zaidi ya Wanawake na Wasichana 1,000 Wafariki Katika Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan
UN: Wanawake na Wasichana 1,025 Wamefariki Katika Tetemeko la Ardhi Mashariki mwa Afghanistan. Ofisi ya Kuratibu Misaada ya Kibinadamu ya Umoja wa Mataifa (OCHA) nchini Afghanistan imetangaza kuwa: Jumla ya wanawake na wasichana 1,025 wamepoteza maisha kutokana na tetemeko la ardhi lililotokea katika maeneo ya mashariki mwa Afghanistan. Taarifa hiyo inasisitiza ukubwa wa athari za kibinadamu, hasa kwa wanawake na watoto, katika tukio hili la maafa ya asili.
-
Al-Bukhaiti: "Vita imeingia katika awamu mpya na wavamizi watalipa gharama kubwa"
Mwanachama wa Ofisi ya Kisiasa ya Harakati ya Ansarullah ametangaza kuwa shambulio dhidi ya kikao cha Serikali ya Yemen huko Sana'a lilivuka mistari miekundu na kwamba vita imeingia katika awamu mpya.
-
Shambulio la Kombora la Yemen Tena Dhidi ya Israel
Vyombo vya habari vya Israel vimeripoti kuwa jeshi la Yemen kwa mara nyingine limeishambulia ardhi ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu kwa kombora.
-
Wayahudi Wanaopinga Uzayuni Wametoa Pongezi kwa Mashahidi wa Mashambulizi ya Israel Dhidi ya Iran
Mayahudi wanao uchukia Uzayuni huko New York, walihudhuria katika Ofisi ya Ujumbe wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran katika Umoja wa Mataifa mjini New York na kutoa heshima zao kwa Mashahidi wa Mashambulizi ya Utawala wa Kizayuni.
-
Waisraeli 24 wauawa na 592 kujeruhiwa katika mashambulizi ya makombora ya Iran katika maeneo yanayokaliwa kwa mabavu
Ofisi ya habari ya Israel imeripoti kuwa, tangu kuanza mashambulizi ya makombora mazito ya Jamhuri ya Kiislamu ndani ya Palestina inayokaliwa kwa mabavu, Wazayuni 24 wameuawa na wengine 592 wamejeruhiwa.