Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- vyombo hivyo vya habari vimekiri kufanyika kwa shambulio hilo na kudai kuwa kombora moja la masafa marefu (ballistic missile) lilirudiwa kufuatiliwa likitoka Yemen.
Hata hivyo, taarifa hizo zilisema kuwa baada ya shambulio hilo, kengele za tahadhari ya mashambulizi ya kombora hazikupigwa.
“Hizam al-Asad,” mjumbe wa ofisi ya kisiasa ya Ansarullah, amesema kuwa hawataacha kuisaidia Gaza.
Amesisitiza kuwa: “Mradi tu utawala wa Kizayuni haujasitisha uvamizi wake na kuondoa mzingiro, tutaendelea kulenga adui wa Kizayuni kwa nguvu zote.”
Baada ya Israel kushambulia Gaza, vikosi vya kijeshi vya Yemen vilianza mashambulizi dhidi ya ardhi inayokaliwa kwa mabavu kwa lengo la kuwaunga mkono Waislamu wenzao wa Gaza.
Mashambulizi hayo yamesababisha hasara kubwa isiyorekebishika katika sekta mbalimbali za kiuchumi za Israel.
Your Comment