Simu
-
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Saudi Arabia Wafanya Mazungumzo kwa Simu Kujadili Hali ya Kanda
Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran, Abbas Araqchi, na mwenzake wa Saudi Arabia, Faisal bin Farhan, wamejadili kwa njia ya simu maendeleo ya hivi karibuni ya kikanda kufuatia hatua za uhasama zilizochukuliwa na Marekani.
-
Rais Pezeshkian: Sera za Kivamizi za Utawala wa Kizayuni Ndizo Chanzo cha Ukosefu wa Usalama katika Eneo
Rais Masoud Pezeshkian amesema sera za uchokozi za utawala wa Kizayuni ndizo chanzo kikuu cha ukosefu wa usalama katika eneo, huku Iran na Serbia zikisisitiza umuhimu wa kuimarisha amani, utulivu na ushirikiano wa pande mbili.
-
Iran na Oman Zasisitiza Umuhimu wa Usalama wa Mlango wa Hormuz Kufuatia Makubaliano ya Hivi Karibuni
Mawaziri wa Mambo ya Nje wa Iran na Oman wamejadili kwa njia ya simu umuhimu wa kulinda usalama wa Mlango wa Hormuz, kuimarisha usalama wa usafiri wa baharini, na kupanua ushirikiano wa pande mbili kufuatia makubaliano ya hivi karibuni kati ya Tehran na Washington.
-
Mazungumzo ya Simu kati ya Trump na Maduro Katikati ya Vitisho vya Kijeshi vya Marekani Dhidi ya Venezuela
Rais wa Marekani, Donald Trump, alifanya mawasiliano ya simu na mwenzake wa Venezuela, Nicolás Maduro, na wakajadili uwezekano wa kufanyika kwa mkutano wa ana kwa ana huko Washington, kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na New York Times. Mawasiliano haya yalifanyika wakati mvutano ukiwa umeongezeka kufuatia hatua ya Marekani kupeleka majeshi yake katika eneo la Karibi na tuhuma za ulanguzi wa dawa za kulevya dhidi ya Maduro-tuhuma ambazo Venezuela huziona kama kisingizio cha kuandaa mabadiliko ya serikali.