Uadilifu
-
Haki na Uadilifu wa Kifamilia katika Mizani ya Riwaya; Tathmini Upya ya Mipaka ya Ndoa ya Muda (Mut’a)
Ndoa ya muda (Mut’a) ambayo Mtume (s.a.w.w) aliihalalisha na Qur’ani ikaithibitisha, kwa msingi wa fiqhi ya Shia ni halali kisheria. Hata hivyo, riwaya zimeweka miongozo ya kimaadili na kijamii inayosisitiza tahadhari katika baadhi ya mazingira.
-
Imani ya Mahdawi: Vipi Iliwafanya Waislamu wa Kishia Kusimama Imara Katika Mitihani Mikubwa ya Ulimwengu wa Kiislamu?
Madhehebu ya Ahlul-Bayt (a.s), likiwa limejengwa juu ya itikadi ya kumwamini Imam Mahdi (a.t.f.s) aliyeahidiwa kwa mataifa yote, linabeba mafundisho yenye utajiri mkubwa kuhusu uadilifu na uokovu. Mafundisho haya yamewafanya Waislamu wa Kishia kubaki imara, thabiti na wenye heshima katika mitihani na misukosuko mikubwa ya ulimwengu wa Kiislamu.
-
Rais wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan:
Uislamu ni mtangulizi wa haki sawa, uadilifu wa kiuchumi na utawala wa haki
Rais wa Baraza la Maulamaa wa Kishia Pakistan amesema kuwa: Uislamu ni mfumo kamili wa maisha ambao ni mtangulizi wa haki sawa, uadilifu wa kiuchumi na utawala wa haki, na mfano bora zaidi wa hayo ni mfumo wa haki wa Imam Ali (a.s) ambao utabaki kuwa kielelezo cha uadilifu na usawa daima.
-
Tukio la “Iran Moyo Mmoja”:
Sheikh Naeem Qassem: Iran Daima Iko Kando ya Muqawama / Mmekuwa Mfano kwa Dunia Nzima
Sheikh Qassem pia aliipongeza Iran ya Kiislamu kwa kusimama kwake kwa ushujaa mkubwa dhidi ya uvamizi wa Marekani na Israel kwa kipindi cha siku kumi na mbili, akisema: “Alhamdulillah, mmeonyesha mfano kwa dunia nzima jinsi ya kupambana na uvamizi, kusimama imara, na kufikia mafanikio makubwa kwa baraka za uongozi wa Imam Khamenei (h.a), umoja wa watu na uaminifu wa wanajeshi wenu shupavu. Ushindi huu utaandikwa katika historia.” Akaongeza kwa kusisitiza: “Tunajua Iran inalipa gharama kubwa kwa kusimama upande wa haki, upande wa muqawama, upande wa Palestina, na upande wa mataifa yote yanayohitaji msaada. Lakini hii ndiyo Iran — mfano wa kujitolea, utukufu na uadilifu — ambayo haidai chochote kwa kusimama na wanyonge. Iran hii imesimama kwa ajili ya utukufu wa ubinadamu.” Sheikh Qassem alizungumzia pia vikwazo vipya dhidi ya Iran, akisema: “Leo tena wameiwekea Iran vikwazo vipya. Je, vikwazo hivi viliwahi kuacha kuwepo? Tangu ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu miaka 46 iliyopita, Iran imeendelea kuwa chini ya vikwazo, lakini kila siku taifa hili limeendelea kung’aa zaidi na kuthibitisha kuwa ni taifa la ukweli na la mapambano.”
-
Arubaini: Jukwaa la Haki, Amani na Uadilifu, na ni Taa ya Uongofu na Jahazi la Uokovu
Historia inaonyesha kuwa jukwaa hili lina mizizi imara katika imani, haki na uadilifu. Lilianza na mtu mmoja au wawili zaidi ya karne kumi zilizopita. Pamoja na changamoto nyingi zilizowakumba waliolipanda, idadi ya washiriki imekuwa ikiongezeka kila mwaka - hasa baada ya Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran.
-
Bondia Muhammad Ali: "Ikiwa unataka kuuelewa Uislamu, basi kwanza jifunze uelewe tukio la Karbala"
Muhammad Ali - Bondia maarufu wa wakati wote alitoa kauli hiyo mwaka 1993 katika Mwezi kama huu wa Muharram ambapo naye alishiriki katika Maombolezo ya Shahada ya Imam Hussein (as).
-
Falsafa ya Maombolezo na Kumbukumbu ya A'shura | Kulinda Haki na Uhuru wa Watu ni Muhimu zaidi kuliko Maisha binafsi
Haki ya mtu binafsi na umma: Imam Hussein alijua kwamba alikuwa akielekea kifo, lakini alikusudia kuonyesha ulimwengu kuwa kulinda haki na uhuru wa watu ni muhimu kuliko maisha binafsi. Maombolezo ya Ashura yanatufundisha kuwa watu wanapaswa kuwa tayari kujitolea, si tu kwa ajili ya nafsi zao, bali kwa ajili ya ustawi wa jamii.