anga
-
Iran Yadungua Ndege ya Marekani Isiyo na Rubani Baada ya Kukiuka Anga ya Nchi Hiyo
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limeripotiwa kudungua ndege ya Marekani isiyo na rubani aina ya MQ-1 Predator baada ya kuingia katika anga ya Iran, tukio lililotajwa kuwa ukiukaji wa makubaliano ya usitishaji mapigano.
-
Kamanda Iran: Tulishambulia Kambi 17 za Marekani na Kufanya Zaidi ya Operesheni 100 Kijeshi
Kamanda wa Ulinzi wa Anga wa Jeshi la Iran kaskazini mwa nchi amedai kuwa Iran ililenga kambi 17 za kijeshi za Marekani katika eneo la kikanda na kufanya zaidi ya operesheni 100 za kijeshi zilizofanikiwa, akisisitiza kuwa mashambulizi hayo yalikuwa sehemu ya “vita vya kikanda” na kwamba mipango ya Marekani na Israel ya kuidhoofisha Iran ilishindwa.
-
IRGC: Ndege za Marekani za RQ-4 na F-35 Zalikimbia Baada ya Kujibiwa na Ulinzi wa Anga wa Iran
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kudungua ndege isiyo na rubani ya Marekani aina ya MQ-9 na kulazimisha ndege ya RQ-4 pamoja na ndege ya kivita ya F-35 kuondoka katika anga ya Iran baada ya kujibiwa na mifumo ya ulinzi wa anga. IRGC imeonya kuwa uvunjaji wowote wa usitishaji mapigano utakabiliwa na majibu makali ya kulipiza kisasi.
-
Kamati ya Uratibu ya Makundi ya Muqawama ya Iraq: Wavamizi wa Marekani Lazima Waondoke
Kamati ya Uratibu ya Makundi ya Muqawama ya Iraq imesisitiza katika taarifa yake kwamba uwepo wa majeshi ya Marekani nchini Iraq ni aina ya uvamizi unaokiuka mamlaka ya taifa hilo, na imetaka kuondoka kwa wanajeshi wa Marekani kutoka ardhi ya Iraq. “Wavamizi wanaendelea kukiuka anga la Iraq; iwe kupitia ndege zisizo na rubani (drones) au kwa kutumia ndege zao za kivita. Hatua hizi zinachukuliwa kuwa tishio kubwa kwa usalama, uthabiti na umoja wa ardhi ya nchi, na ni uvamizi wa wazi dhidi ya mamlaka na heshima ya dola ya Iraq.”
-
Waziri wa Ulinzi wa Pakistan, Khawaja Muhammad Asif: "Pakistan haitasita kufanya mashambulizi ya anga ndani ya Afghanistan ikiwa itahitajika"
Khawaja Asif, Waziri wa Ulinzi wa Pakistan, ameeleza kuwa Islamabad haitakosa kufanyia mashambulizi ya anga ndani ya Afghanistan ikiwa itaona ni lazima, chini ya utawala wa Taliban. Alidai kwamba makundi ya silaha yanayofanya operesheni kutoka ardhi ya Afghanistan yanaingiliana katika mashambulizi dhidi ya Pakistan.
-
Iraq yakataa kuruhusu matumizi ya anga lake kwa mashambulizi dhidi ya Iran
Tamko la Iraq linaonyesha kuwa Iraq inalinda mamlaka yake na haitaki kuhusishwa na migogoro ya kijeshi katika eneo hilo, ikisisitiza sera ya kudumisha usalama na utulivu wa kikanda.
-
Maariv: Utoaji wa Onyo la Mabomu la Iran Linasababisha Washington Kusogeza Mazungumzo
Gazeti la Kizayuni Maariv linaripoti kwamba onyo la Iran kuhusu jibu la makali la kijeshi limechochea Washington kurudisha nyuma chaguo la kijeshi na kusogeza hatua kuelekea mazungumzo. Iran kwa sasa inatumia sera ya ukosefu wa uhakika wa kimkakati ili kuimarisha uwezo wake wa kuzuia mashambulizi na kuepuka mgongano mpya, huku ikipata uzoefu mkubwa katika kuvuka mifumo ya ulinzi wa anga ya Israeli na Marekani.
-
Sayyid Ali Khomeini: “Kama Ubalozi wa Marekani usingelivamiwa, leo tusingekuwa na Makombora wala ishati ya nyuklia"
Akiisisitizia kauli kwamba “uvamizi wa ubalozi wa Marekani uliimarisha uhuru wa Iran,” alisema: “Kama tukio hilo lisingetokea, leo hii Jamhuri ya Kiislamu isingekuwepo, na nchi yetu isingepata teknolojia ya makombora na nishati ya nyuklia, kwani Marekani ilikuwa inapinga maendeleo haya.”
-
Uchokozi wa Israel: Rais wa Iran aitaka Iraq kulinda mipaka yake, anga
Picha ya mchanganyiko inawaonyesha Rais wa Iran Masoud Pezeshkian (Kulia) na Waziri Mkuu wa Iraq Muhammad Shayya al-Sudani.