kushambulia
-
Ayatollah Jawadi Amoli: Iran haijawahi kuwa ya kwanza kushambulia na haitampa mvamizi usalama
Kiongozi wa kidini Ayatollah Abdullah Jawadi Amoli amesisitiza kuwa wananchi wa Iran hawajawahi kuwa wa kwanza kuanzisha mashambulizi dhidi ya wengine, na kwamba hawatampa usalama wala nafasi yoyote mvamizi yeyote, akisisitiza umuhimu wa kulinda usalama, utulivu wa nchi na umoja wa kitaifa.
-
Marekani yaonya China au Urusi huenda wanasaidia Iran kushambulia malengo ya Marekani
Maafisa wa Marekani wana wasiwasi kuwa China au Urusi huenda wanatoa msaada kwa Iran katika mashambulizi yake dhidi ya malengo ya Marekani, kwa mujibu wa ripoti ya Wall Street Journal. Ripoti hiyo pia inasema Iran sasa inatumia makombora yanayoweza kuendeshwa wakati wa kuruka na yanayosafiri kwa kasi kubwa sana, jambo linalofanya ulinzi wa anga kuwa mgumu zaidi. Hatua hiyo imeongeza hofu kuhusu uwezo wa Iran wa kupenya mifumo ya ulinzi na kuongeza hatari ya mzozo mpana zaidi katika eneo hilo.
-
IRGC Yathibitisha kushambulia kwa kushtukiza kituo cha uongozi wa operesheni za Marekani eneo la Al-Tanf nchini Syria
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limetangaza kuwa limefanya shambulio la kushtukiza dhidi ya kituo cha uongozi wa operesheni maalumu kinachodaiwa kutumiwa na majeshi ya Marekani katika eneo la Al-Tanf nchini Syria, likisema hatua hiyo ni majibu ya mashambulizi yaliyosababisha vifo vya wanajeshi wa Iran.
-
IRGC yatangaza awamu ya pili ya Operesheni "Nasr 2"; yadokeza kushambulia vituo vya mawasiliano na makazi ya wanajeshi wa Marekani Bahrain
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu (IRGC) limedai kuwa katika awamu ya pili ya Operesheni "Nasr 2" lililenga maghala ya silaha, kituo cha mawasiliano ya satelaiti na jengo la makazi ya wanajeshi wa Marekani katika Kambi ya Al-Juffair nchini Bahrain.
-
Hezbollah Yatangaza Mashambulizi 22 Dhidi ya Vikosi vya Israel Kusini mwa Lebanon
Hezbollah imesema imefanya operesheni 22 za kijeshi kwa kutumia makombora, ndege zisizo na rubani na mizinga dhidi ya vikosi vya Israel kusini mwa Lebanon, ikidai kuharibu magari ya kijeshi, kulenga vituo vya kijeshi na kulazimisha ndege ya Israel ya aina ya Hermes 450 kuondoka katika anga la Lebanon.
-
IRGC Yathibitisha Kushambulia Makao Makuu ya Kikosi cha Tano cha Jeshi la Wanamaji la Marekani Bahrain Kwa Kutumia Droni
Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC) wamedai kufanya shambulizi la ndege zisizo na rubani dhidi ya makao makuu ya Kikosi cha Tano cha Jeshi la Wanamaji la Marekani nchini Bahrain, katika kile walichokiita kujibu mashambulizi dhidi ya maeneo ya kusini mwa Iran.
-
Daesh wabeba jukumu la shambulio dhidi ya doria ya wanamgambo wa Jolani
Daesh wametekeleza tukio la kushambulia doria inayohusiana na idara ya forodha ya Serikali ya Jolani na kuua watu wawili.