Maneno haya ni wito wa kutuweka kwenye mstari wa Ucha Mungu, uwajibikaji wa nafsi, na kujiepusha na dhambi kwa kutambua kuwa hakuna kisichojulikana mbele ya Mwenyezi Mungu (swt).
Katika uwanja wa kisiasa, kauli hii inaweza kumaanisha kuwa taifa au jamii halipaswi kuruhusu kushambuliwa, kupuuzwa au kudhulumiwa na adui wa ndani au wa nje, bali lazima ichukue hatua za kulinda maslahi yake kwa ujasiri.