maombolezo
-
Mkutano wa Tatu wa Kitaaluma kuhusu Maombolezo na Desturi za Kidini; Kusisitiza nafasi ya kihadhari ya Hay’a katika jamii na familia
Hujjatul-Islam wal-Muslimin Babakhani pia alisisitiza nafasi ya wanawake katika hay’a na kusema: “Tangu kuundwa kwa hay’a, wanawake wamekuwa mstari wa mbele katika uongozi wa kitamaduni na kidini - kuanzia Bibi Fatima az-Zahra (a.s) na Bibi Zaynab (a.s) hadi leo - na wametoa mchango mkubwa katika kuhifadhi na kueneza utamaduni wa hay’a. Uwepo wao umeleta athari kubwa katika kufundisha mafundisho ya dini na kuonyesha kwa jamii fadhila za Ahlul-Bayt (a.s).”
-
Haj Mirza Baqer; Mweka Waqfu wa Maukufu Maarufu ya Fatimiyya huko Qom
Miongoni mwa maukufu (mambo yaliyowekwa wakfu) machache ya Qom yaliyosajiliwa kwa nia ya kuadhimisha maombolezo ya Bibi Fatima Zahra (a.s) na ambayo bado yanaendelea kutumika hadi leo, ni maukufu (yaliyowekwa na Haj Mirza Baqer katika miaka ya ishirini ya karne iliyopita.
-
Darsa Fupi na Muhimu Katika Muktadha wa Maombolezo ya Bibi Fatimah az-Zahra (a.s) kuhusu "Fadhila na Siri za Tasbihat az-Zahra (a.s) na Ayatul Kursi"
Imam al-Baqir (a.s.) amesema: “Anayesema Tasbih ya Fatimah az-Zahra (a.s.) kisha akaomba maghfirah, atasamehewa. (Tasbih hiyo inaposomwa na mja) Ni mia moja kwa ulimi wake, lakini ni elfu moja katika mizani.”
-
Majlisi ya Kumbukumbu ya Shahada ya Sayyid Hassan Nasrallah Kufanyika Beirut
Katika hafla hiyo: Mzungumzaji mkuu atakuwa Sheikh Muhammad Sadiq.
-
Baraza la Utamaduni la Ubalozi wa Iran Nairobi Latuma Salamu za Rambirambi kwa Kumbukumbu ya Kifo cha Mtume Muhammad (s) na Shahada ya Imam Hassan a.s
Siku hii pia inakumbusha shahada ya Imam Hassan (a.s), Imam wa pili katika Ahlul-Bayt (a.s), aliyefahamika kwa msimamo wake wa amani na kujitolea kwake kwa ajili ya haki. Kifo chake ni alama ya mapambano ya kudumu kwa ajili ya uadilifu na uongofu.
-
Katibu Mkuu wa Baraza la Maimamu wa Kishia Pakistan:
Kukandamiza waombolezaji wa Imam Hussein (a.s) Punjab ni kitendo cha woga na kinyume na haki za kiraia
Katibu Mkuu wa Baraza la Maimamu wa Kishia nchini Pakistan, Hujjatul-Islam Shabir Hassan Meesami, amelielezea hatua ya Serikali ya Punjab ya kuwashughulikia kwa nguvu waombolezaji wa Imam Hussein (a.s) na kufungua kesi za kisheria dhidi yao kuwa ni kitendo cha woga, akitaka kusitishwa mara moja kwa kukamatwa kiholela na kuachiliwa kwa wote waliokamatwa.
-
Iran | Kesho ni Siku ya Maombolezo ya Kitaifa Nchini Iran / Idadi ya Waliopoteza Maisha Yafikia 28
Baada ya tukio la kusikitisha katika Bandari ya Shahid Rajaei lililosababisha vifo vya makumi ya raia wapenzi wa Iran, Baraza la Mawaziri limetangaza kuwa kesho kutakuwa na maombolezo ya kitaifa kote nchini.