shughuli
-
Taliban Wamefunga Kituo cha Kielimu na Kitamaduni cha Imam Hussein (a.s) Jijini Kabul
Kituo cha Kielimu na Kitamaduni cha Imam Hussein (a.s) kilihesabiwa kuwa miongoni mwa vituo hai vya kitamaduni vya Waislamu wa Kishia katika magharibi mwa Kabul. Kufungwa kwake kumeibua hisia na malalamiko miongoni mwa wakazi wa eneo hilo na wanaharakati wa kitamaduni, ambao wameeleza wasiwasi wao kuhusu mustakabali wa shughuli za kielimu na kitamaduni za jamii hiyo chini ya utawala wa sasa.
-
Kongamano la Waombolezaji wa Kike wa Fatimiyyah Kufanyika Mjini Qom - Iran
Wanawake waumini jijini Qom watafanya matembezi ya maombolezo hadi kwenye kaburi la Shahidi Asiyejulikana katika chuo cha Jami‘atu-z-Zahra (a), wakiomboleza kumbukumbu ya shahada ya Bibi Fatima Zahra (a), Mama wa Maimamu wa Ahlul-Bayt (as).
-
Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Ahlul Bayt (a.s) Akutana na Imam wa Isfahan | Asisitiza Upanuzi wa Shughuli za Dini
Akizungumza kuhusu ziara yake Ispahan, Ayatullah Reza Ramadhani alikutana na Ayatullah Sayyid Yusuf Tabatabai-Nejad na kutoa ripoti kuhusu programu za mabadiliko na shughuli za kimataifa za Jumuiya ya Kimataifa ya Ahlul Bayt (a.s).
-
Shukrani za Ayatollah Nouri Hamadani kwa jitihada za Ofisi ya Vikundi vya Misikiti katika shughuli za Qur’an / Ihitaji uwepo mkubwa zaidi wa vijana katika Misikiti.
Kiongozi wa kiitikadi wa Mashia alisema kuwa: ‘Msikiti usio na vijana hauwezi kustawi, na uwepo wa vijana katika misikiti ni wa thamani sana.’ Alisisitiza: ‘Ninashukuru na kupongeza jitihada za Vikundi vya Utamaduni na Sanaa vya Misikiti katika shughuli za Qur’an na uhai wa misikiti, na nina matumaini uwepo wa vijana katika misikiti utakuwa mkubwa zaidi.
-
Uzinduzi wa Mfumo wa Kielelezo cha Kujadiliana na Tafsiri za Qur’ani / Ayatollah Makarem:Teknolojia Mpya Iwe Kwenye Huduma ya Qur’ani na AhlulBayt(as)
Ayatollah Makarem Shirazi, mmoja wa maraja’ wa kiislamu, akisisitiza umuhimu wa kueneza habari za mafanikio ya kisayansi, alisema: “Moja ya mahitaji muhimu ya leo ni kuwafahamisha watu. Kuna shughuli nyingi zenye thamani zinafanyika, lakini taarifa zake ni chache. Vyombo vya habari, redio, televisheni na mashirika ya habari vinapaswa kusambaza maendeleo haya ili wananchi waone kiwango cha maendeleo ya teknolojia mpya katika sekta ya elimu ya dini.”