Je, inaweza kusemwa kwamba kuna jua lakini hakuna mwanga?
Kuumbwa kwa ulimwengu ni matokeo ya sifa za Mungu. Mungu ni mjuzi wa yote. Mungu ni muweza. Mungu ndiye muumbaji. Mungu ni mwenye hekima. Mungu ni mwema. Mungu ni mkarimu na…
Ikiwa Mungu hangeumba ulimwengu huu na uzuri huu, sifa za Mungu zingebaki zimefichwa.
Iwapo mtu miongoni mwetu ana uwezo wa kuumba kitu, lakini hakuumba, tunamwambia kwamba unaweza kuumba hiki kitu, kwa nini usitumie uwezo wako huu? Je, si hivyo? Basi kwa nini tusimpe Mungu haki hii ya kuonesha uwezo wake kwa wengine.
Kwa hivyo, Mungu aliumba, kwa sababu Yeye ndiye Muumba, Anaweza, ni Mwenye hekima, ni Mwingi wa rehema na Mkarimu.
Kwa hiyo, kila kitu ambacho kina uwezo wa kuwepo, Mungu anakiumba. Kwa nini? Kwa sababu ya sifa alizonazo Mungu.
Chanzo: alanwaralmunirah