28 Desemba 2024 - 20:02
Uungaji Mkono kwa Gaza huko Brighton, Uingereza, kwa kuinua Bendera ya Palestina juu ya nyumba

Watetezi wa Palestina ambao tangu kuanza kwa vita huko Ghaza wameonyesha hasira na vipingamizi vyao dhidi ya jinai za utawala haram wa Kizayuni kwa kufanya maandamano katika Miji mbalimbali ya Uingereza, safari hii walijaribu kudhihirisha na kufikisha sauti ya (maandamano yao) vipingamizi vyao kwa njia ya mfano (kivitendo).

Kwa mujibu wa Shirika la Habari la Kimataifa la Ahl al-Bayt (a.s) - ABNA - Idadi kadhaa ya wafuasi wa Palestina huko Brighton, Uingereza, waliendelea na maandamano dhidi ya jinai za kinyama za utawala haram wa Kizayuni dhidi ya Ghaza na kuonyesha mshikamano wao kwa wananchi wa Palestina, kwa kupeperusha Bendera ya Palestina kutokea majumbani mwao (na katika majumba yao).

Vuguvugu hili la maandamano, ambalo lilifanyika Ijumaa ya mwisho ya 2024, lilionekana huku Bendera za Palestina zikiwa zimeinuliwa juu kutoka kwenye madirisha ya nyumba nyingi katika moja ya Barabara kuu za Mji wa Brighton.

Watetezi wa Palestina ambao tangu kuanza kwa vita huko Ghaza wameonyesha hasira na vipingamizi vyao dhidi ya jinai za utawala wa Kizayuni kwa kufanya maandamano katika miji tofauti ya Uingereza, safari hii walijaribu kupaza sauti zao za kupinga kitendo cha serikali hiyo kutojali hali mbaya na kuleta maafa ya kibinadamu na mauaji ya kimbari huko Gaza, kupitia njia ya mfano (kwa kuonyesha upingaji wao kivitendo na kiishara).

Serikali ya Uingereza bado haijataja jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya Ghaza kuwa ni mauaji ya kimbari.