23 Oktoba 2025 - 12:59
Tangazo la Nafasi za Masomo ya Kidini katika Hawzat Imam Ridha (a.s) – Ikwiriri, Rufiji kwa Mwaka wa Masomo 2025–2026 +Audio

Hawzat Imam Ridha (a.s) | “Elimu ni nuru, na nuru hiyo ni ya Allah (s.w.t)”

Tangazo la Nafasi za Masomo ya Kidini katika Hawzat Imam Ridha (a.s) – Ikwiriri, Rufiji kwa Mwaka wa Masomo 2025–2026

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Hawzat Imam Ridha (a.s) - Chini ya Taasisi ya Kiislamu ya Hujjatul Asr Society of Tanzania - Ikwiriri – Rufiji, Mkoa wa Pwani, inatumia Nafasi hii kuwatangazieni nafasi za masomo ya kidini kwa mwaka wa masomo 2025 – 2026. Waislamu wote wanaopenda kujifunza elimu za dini ya Kiislamu chini ya mwongozo wa Ahlul-Bayt (a.s) wanakaribishwa kuomba nafasi katika Hawzat hii Tukufu.

 Tarehe ya Usaili: Jumamosi, 22 Novemba 2025 - Mahali: Makao Makuu ya Hawzat Imam Ridha (a.s), Ikwiriri – Rufiji.


Vigezo vya Mwombaji: Awe ni Muislamu mwenye nia ya dhati ya kusoma elimu za dini. Awe amemaliza angalau elimu ya sekondari (O-Level) au sawa na hapo. Awe tayari kufuata nidhamu na kanuni za Hawza.

Faida za Masomo:

1_Mafunzo ya kidini kwa kina katika mazingira ya kiroho.

2_Miongozo na malezi bora kutoka kwa walimu wenye sifa.

Tangazo la Nafasi za Masomo ya Kidini katika Hawzat Imam Ridha (a.s) – Ikwiriri, Rufiji kwa Mwaka wa Masomo 2025–2026


Kwa maelezo zaidi, wasiliana na:
📞 Simu: [+255 787 103 888]

Hawzat Imam Ridha (a.s)
“Elimu ni nuru, na nuru hiyo ni ya Allah (s.w.t)”

Your Comment

You are replying to: .
captcha