22 Desemba 2025 - 21:28
Iran Yatuma Makundi Mawili ya Kijeshi Baharini Kulinda Meli Zake

Wachambuzi wa kimataifa wanasema kuwa hatua hii inaongeza mvutano kati ya Tehran na Washington, huku ikionyesha hatari zinazoongezeka kwa usalama wa usafirishaji wa baharini.

Shirika la Habari la Kimataifa la Ahlul-Bayt (as) -ABNA- Tehran - Jeshi la Majini la Iran limezituma Tasking Groups 103 na 104 katika operesheni baharini, lengo likiwa ni kulinda meli zinazohusiana na Iran zinazofanya kazi katika maji ya kimataifa.


Hatua hii imechukuliwa kufuatia kile Tehran kinachokieleza kama vitendo vya Marekani vya kunyang’anya au kukamata meli zinazohusiana na Iran. Vyanzo vya kijeshi vya Iran vinasema kuwa makundi hayo mawili ya kijeshi kwa sasa yanaelekea katika eneo la bahari karibu na South Africa, jambo linaloashiria kuongezeka kwa uwepo wa kijeshi wa Iran katika njia muhimu za biashara za baharini.


Wachambuzi wa kimataifa wanasema kuwa hatua hii inaongeza mvutano kati ya Tehran na Washington, huku ikionyesha hatari zinazoongezeka kwa usalama wa usafirishaji wa baharini. Hii ni hatua nyingine inayoonyesha jinsi mzozo wa kisiasa na kijeshi kati ya Iran na Marekani unavyoweza kuathiri njia kuu za biashara za kimataifa.

Tags

Your Comment

You are replying to: .
captcha