Ujasiri
-
Katika ujumbe kwa Mkutano wa Mwaka wa Umoja wa Vyama vya Wanafunzi wa Kiislamu barani Ulaya; Kiongozi wa Mapinduzi:
Hitaji kuu la dunia leo ni mfumo wa haki wa kitaifa na kimataifa wa Kiislamu / Shambulio la Marekani lilishindwa mbele ya ujasiri wa vijana wa Iran
Ayatollah Khamenei, katika ujumbe wake kwa Mkutano wa 59 wa Mwaka wa Umoja wa Vyama vya Wanafunzi wa Kiislamu barani Ulaya, amesisitiza kuwa sababu kuu ya msukosuko na wasiwasi wa madhalimu wafisadi si suala la nyuklia, bali ni kuinuliwa kwa bendera ya kupinga mfumo usio wa haki na utawala wa mabavu wa mfumo wa ubeberu duniani, pamoja na mwelekeo wa Iran ya Kiislamu kuelekea kujenga mfumo wa haki wa kitaifa na kimataifa wa Kiislamu.
-
Kinyume na madai ya Taliban; Umoja wa Mataifa waripoti kuongezeka kwa shughuli za ISIS nchini Afghanistan
Umoja wa Mataifa katika tathmini yake ya hivi karibuni ya kiusalama umetangaza kuwa ISIS Khorasan, kinyume na madai ya Taliban, si tu kwamba haijadhibitiwa, bali kwa kubadili mbinu na kuvutia wapiganaji wapya, imepanua shughuli zake hadi katika miji mikubwa ya Afghanistan.
-
Ni vipi Fatima Zahra (a.s) Alikuwa Mpenzi na Mpendwa Zaidi Katika Maisha ya Ali (a.s)?
Katika baadhi ya nyakati, mtu humtambulisha nafsi yake kwa kutaja nasaba yake na watu wakubwa. Hivyo ndivyo alivyofanya Amirul-Mu'minin Ali (a.s) katika mojawapo ya khutba zake baada ya kurejea kutoka vita vya Nahrawan. Ali (a.s) alisema: “Mimi ni mume wa Bibi Batul, Bibi wa wanawake wa ulimwengu, Fatima aliye mchamungu, msafi, mtukufu, mwongofu, mpendwa wa Mpenzi wa Allah, bora wa mabinti wake na mchanga wa roho ya Mtume wa Allah (s.a.w.).” Kutaja kwa Imam Ali (a.s) daraja la juu la Bibi Zahra (a.s) baada ya kujinasabisha na mwanamke huyu mtukufu ni kusisitiza nafasi kuu ya bibi huyu mbele ya mtu mkubwa kama Ali (a.s).
-
Hakim: Kimya mbele ya uvamizi wa Israel hakikubaliki
Sayyid Ammar Hakim amesema kuwa ujasiri wa hali ya juu na dharau ya wazi ya utawala wa Kizayuni katika kuvamia nchi za Kiarabu na Kiislamu, na kutenda jinai za kila siku dhidi ya watu wa Ukanda wa Gaza, Ukingo wa Magharibi, Syria, Lebanon, Yemen, Iran na Qatar ni jambo ambalo kimya dhidi yake hakikubaliki.
-
Hamza(ra), Bendera ya Kwanza ya Uislamu
Hamza bin Abdulmuttalib (ra), ami yake Mtume wa Uislamu(saww), anajulikana kama Bendera ya kwanza ya Uislamu. Kwa ujasiri na kujitolea kwake katika kumtetea Mtume na mafundisho ya Kiislamu, alicheza nafasi muhimu katika kueneza Uislamu. Hamza hakuwa tu shujaa katika uwanja wa vita, bali pia alikuwa mfano na mlinzi wa Waislamu, daima akiwa upande wa Mtume na kwa msimamo wake, alitia nguvu na matumaini katika nyoyo za waumini.
-
Mimbari ya Imam Hussein (as) - Nchini Malawi | "Tofauti kati ya Mtu anayemjua Imam Hussein (AS) na Asiyemjua Imam Hussein (as)"
Sheikh Abdul Rahman Kachere: "Mtu anayemfahamu Imam Hussein (AS) daima ni jasiri katika kukabiliana na dhulma".Kumjua vizuri Imam Hussein (as) kutawafanya watu wa mataifa mbalimbali kumpinga adui na dhalimu, na kutambua njama za adui na dhalimu dhidi ya mataifa yao, na kuwa tayari kupambana kwa ajili ya kuinusuru Haki, kwa ajili ya kuondoa uistikbari, dhulma na unyonyaji wa mfumo mpya wa ukoloni unaoitwa: Ukoloni mambo leo.
-
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran:
"Kila afisa wa Kijeshi au Mwanasayansi wa Nyuklia wa Iran anayeuliwa Kigaidi, kuna wengine mia moja nyuma yake walioko tayari kuchukua nafasi yake"
Abbas Araqchi alisema: "Tofauti na utawala wa Kizayuni, Iran haitaficha kamwe hasara zake na inajivunia Mashahidi wake kama vielelezo vya ujasiri. Taifa la Iran litasimama kidete dhidi ya yeyote anayejaribu kuliamulia mustakabali wake hadi tone la mwisho la damu".
-
Jerry, Mwendesha kipindi wa Al Jazeera: "Ikiwa uchokozi wa Marekani haungejibiwa na Iran, Marekani ingeenda mbele zaidi na kuingilia vita"
Ujasiri huu wa Iran ulikuwa wa kuzuia hamu ya Marekani ya kutaka kuingilia kati vita vya israel dhidi ya Iran - ili kuisaidia na kuiokoa Israel (iliyokuwa imelemewa na vita).
-
Maana ya Maneno ya Ayatullah Ustadh Abdullah Jawadi Amuli kwamba: “Rudisha jiwe, kule lilipotoka”
Katika uwanja wa kisiasa, kauli hii inaweza kumaanisha kuwa taifa au jamii halipaswi kuruhusu kushambuliwa, kupuuzwa au kudhulumiwa na adui wa ndani au wa nje, bali lazima ichukue hatua za kulinda maslahi yake kwa ujasiri.
-
Hadithi ya Shetani na Mwanadamu:
"Siri ya Muda wa Shetani Kuishi: Kwa Nini Mwenyezi Mungu Alimpa Shetani Muda Mrefu wa Kuishi?
Tangu wakati huo ambapo Shetani aliasi na kukataa kumsujudia Adam (a.s), mzozo wa kihistoria kati yake na Mwanadamu ulianza; mzozo ambao unaendelea hadi leo hii. Lakini swali muhimu ni hili: Kwa nini Mwenyezi Mungu alimpa adui huyu katili (Shetani) muda mrefu wa kuendelea kuishi na kujaribu na kuwapoteza watoto wa Adam (Wanadamu)?!. Nakuletea Hadithi nzuri na yenye mazingitio ndani yake kuhusu Shetani na Mwanadamu, na utaijua sababu na siri ya Ruhusa ya Mwenyezi Mungu kwa Shetani ili aendelee kuishi kwa muda mrefu.
-
Sehemu ya Fadhila za Kipekee za Imam Ali (a.s):
Imam Ali (a.s) ni Mtu wa Kwanza kuzaliwa ndani ya Msikiti na Kuuliwa ndani ya Msikiti
Imam Ali (a.s), Maisha yake yote yalikuwa ni Maisha ya kuweka uthabiti na kuimarisha nguzo na misingi ya Uislamu, pia kujitolea muhanga kwa kitu ghali na chenye thamani kubwa, ili kuhakikisha neno la Mwenyezi Mungu linakuwa juu, na neno la makafiri linakuwa chini.