Waumini
-
Maulana Sheikh Hemed Jalala Aendelea kuimarisha Umoja wa Waislamu Kupitia Ziara ya Kidini Nchini Tanzania
Katika moja ya sehemu za ziara yake, Maulana Sheikh Hemed Jalala alitembelea Mkoa wa Kigoma, ambapo alipokelewa kwa mapokezi mazuri kutoka kwa waumini na viongozi wa dini wa eneo hilo. Moja ya matukio muhimu katika ziara hiyo ni kukutana kwake na Sheikh wa Mkoa wa Kigoma (BAKWATA), Samahat Sheikh Hassan Kiburwa, katika ofisi za BAKWATA Mkoa wa Kigoma, ambapo viongozi hao wawili walifanya mazungumzo ya kina kuhusu maendeleo ya Uislamu, umoja wa Waislamu, na namna bora ya kuimarisha harakati za kidini nchini.
-
Waumini wa Kabul Waadhimisha Arubaini ya Imam Hussein (a.s) Wakihoji Vikwazo vya Safari za Mahujaji (Mazuwwari) wa Afghanistan
Sambamba na kuwadia kwa siku ya Arubaini ya Imam Hussein (a.s), hafla ya kuadhimisha siku hii ilifanyika katika Kituo cha Fiqhi cha Maasemamu Watakatifu (a.s) upande wa magharibi mwa jiji la Kabul. Washiriki, sambamba na kufanya maombolezo kwa ajili ya Imam Hussein (a.s), walitoa malalamiko makali dhidi ya ukosefu wa uratibu wa kisiasa na kisheria ambao mwaka huu uliwazuia waumini wengi wa Afghanistan kusafiri kwa wingi kwenda Karbala.
-
Ubaguzi Dhidi ya Wafuasi wa Shia Nchini Punjab: Serikali Yatumia Shinikizo na Vitisho Kukomesha Maandamano ya Arbaeen Husseini (as)
Serikali ya Punjab imewaita wamiliki wa vibali vya kufanya maombolezo, waandaaji wa vituo vya kutoa huduma za bure (maisha ya Sadaka) na wajumbe wa kamati za ulinzi, na kuwashinikiza watangaze rasmi kujitenga na matembezi ya Arbaeen kuelekea Karbala.
-
(Muqawamah) Kusimama dhidi ya Ubeberu ni Fahari ya Mataifa ya Waumini
"Kazi yetu kuu ni kuinua bendera ya Qur’an ili kwa kueneza mtindo sahihi wa maisha, jamii ya Kiqur’ani iweze kuundwa. Ikiwa nchi za Kiislamu zitaifuata Qur’an, zitauweza kuwalazimisha maadui kurudi nyuma"
-
Thawabu na Faida Kuu za Kuswali Sala ya Jamaa | Madrasat Hazrat Zainab (sa) Kigamboni, Dar-es-Salam kama mfano hai katika kudumisha Sala za Jamaa
Sala ya Jamaa ni Kinga dhidi ya Shetani. Na Mtume wetu Muhammad (s.a.w.w) alisema: فإنَّما يأكلُ الذئبُ منَ الغنمِ القاصيةَ / “Hakika mbwa mwitu humla Kondoo aliyejitenga.”