gazeti
-
Washington Post: Idadi halisi ya wanajeshi wa Marekani waliouawa katika vita na Iran ni kubwa kuliko ilivyoripotiwa na Pentagon
Maafisa wenye taarifa kuhusu idadi kubwa zaidi ya vifo wameeleza wasiwasi wao kuhusu kutorekodiwa kwa baadhi ya vifo hivyo katika hifadhidata ya umma ya Pentagon. Wizara ya Vita ya Marekani pia imekataa kujibu maswali ya Washington Post kuhusu sababu ya tofauti hiyo.
-
Waandishi Watatu Wafunguliwa Kesi Dhidi ya Hegseth na Pentagon kwa Madai ya Udhibiti wa Vyombo vya Habari
Waandishi watatu wa gazeti la kijeshi la Stars and Stripes wamefungua kesi katika mahakama ya shirikisho dhidi ya Waziri wa Ulinzi wa Marekani Pete Hegseth na maafisa wengine wa Pentagon, wakidai kuwa walifukuzwa kazi kwa kulinda uhuru wa vyombo vya habari na kuripoti kuhusu hali mbaya ya wafanyakazi wa manowari ya ndege ya USS Abraham Lincoln.
-
New York Times: “Msidharaueni Houthi Kamwe” na Kumbukeni Silaha Zao
Gazeti la New York Times limeonya dhidi ya kuendelea kuwapuuza Houthi wa Yemen, likisisitiza kuwa wamegeuka kuwa nguvu muhimu ya kikanda yenye uwezo wa kuathiri hesabu za vita na amani, huku eneo la Yemen la kimkakati likiwapa uwezo wa kutumia njia za baharini kama silaha ya kimkakati.
-
Marekani Yazidiwa na Madeni ya Dola Trilioni 40, Huku Iran Ikipinga Vikali “Vita vya Kiuchumi” vya Trump
Marekani imefikia deni la taifa la zaidi ya dola trilioni 40 kwa mara ya kwanza, huku Iran ikikosoa vikali sera za vikwazo na “vita vya kiuchumi” vya Trump, ikisema hatua hizo haziwezi kulazimisha Tehran kujisalimisha.
-
Kura ya Maoni Marekani Yawapa Demokrasia Nafasi, Mvutano wa Hormuz Waongezeka huku Ripoti Zikionya Kuhusu Akiba ya Makombora ya Marekani
Kura mpya ya maoni imeonyesha kuwa wapiga kura wa Marekani sasa wanawaamini zaidi chama cha Democratic katika masuala ya uchumi kuliko Republican. Wakati huo huo, mvutano katika Mlango wa Hormuz unaendelea kuongezeka kutokana na mapendekezo mapya ya Iran, huku ripoti zikieleza kuwa jeshi la Marekani lilitumia sehemu kubwa ya makombora yake ya masafa marefu katika vita dhidi ya Iran.
-
Kura ya Maoni: Wamarekani Wengi Waamini Mzozo Dhidi ya Iran Haujafanikisha Malengo
Kwa mujibu wa gazeti la The Hill, kura mpya ya maoni imeonyesha kuwa Wamarekani wengi wanaamini kuwa mzozo dhidi ya Iran haujafanikisha malengo yaliyokusudiwa
-
The Guardian: Mtandao wa X Watuhumiwa Kuwazuia Wakosoaji wa Serikali ya Saudi Arabia
Gazeti la The Guardian linaripoti kuwa mtandao wa kijamii wa X umezuia zaidi ya akaunti 60 zinazoukosoa serikali ya Saudi Arabia kwa watumiaji walioko ndani ya nchi hiyo, hatua iliyozua ukosoaji kutoka kwa watetezi wa haki za binadamu.
-
Financial Times: Trump Akwama Kati ya Kuongeza Vita na Iran au Kukubali Makubaliano
Gazeti la Financial Times linaripoti kuwa Rais wa Marekani Donald Trump anakabiliwa na chaguo gumu kati ya kuongeza mzozo na Iran au kukubali makubaliano yanayozingatia masharti ya Tehran, hali inayoonyesha kupungua kwa nafasi za Washington katika sera yake dhidi ya Iran.
-
Haaretz: Enzi ya utawala wa Marekani na zama za Netanyahu zimefikia mwisho
Gazeti la Kiebrania la Haaretz limesema kuwa baada ya vita vya hivi karibuni, Iran imekaribia zaidi nafasi ya kuwa nguvu kuu ya kikanda katika Ghuba ya Uajemi, huku likidai kuwa enzi ya utawala wa Marekani, mfumo wa dunia wa upande mmoja na zama za Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu zimefikia mwisho.
-
Gazeti la Kizayuni: Israel Yakabiliwa na Wimbi Lisilo la Kawaida la Vikwazo vya Kimataifa
Gazeti la Yedioth Ahronoth limesema utawala wa Kizayuni wa Israel umekumbwa na ongezeko kubwa la vikwazo na shinikizo la kimataifa tangu Oktoba 2023, huku baadhi ya viongozi wake wakikabiliwa na hati za kukamatwa na marufuku ya kuingia katika nchi mbalimbali.
-
Onyo la Vyombo vya Habari vya Kihibri Kuhusu Kuongezeka kwa Ujasusi kwa Iran katika Ardhi Zinazokaliwa
Gazeti la Israel Hayom limeripoti ongezeko la Wayahudi wa Israeli, hasa Wayahudi wa Orthodox (Haredi), kushirikiana kimaslahi na Iran. Shabak linafuatilia hali hii kwa tahadhari, na baadhi ya watu tayari wamekamatwa wakihusishwa na ujasusi.
-
Ripoti ya The New York Times kuhusu kesi ya Jeffrey Epstein: Mtandao wa ushawishi bila uwajibikaji
Ripoti ya gazeti la The New York Times inafichua jinsi Jeffrey Epstein alivyokuwa na mtandao mkubwa wa wanasiasa, wafanyabiashara, na watu mashuhuri waliokuwa wakiufaidi ushawishi wake bila uwajibikaji. Licha ya ufichuzi huu mkubwa, hakuna mmoja kati ya watu hawa aliyehukumiwa, jambo linaloongeza kutoaminiana kwa umma na kuibua uvumi kuhusu vifo vya Epstein gerezani mwaka 2019.
-
Le Figaro yafichua: Vita halisi vya Israel dhidi ya Iran vinaendelea katika mitandao ya kijamii!
Le Figaro yafichua kuwepo kwa vita vya kisaikolojia vya Israel dhidi ya Iran kupitia mitandao ya kijamii. Ripoti inasema lengo ni kusukuma simulizi ya kubadilisha utawala sambamba na vitisho vya kijeshi. Akaunti bandia, maudhui ya AI, hashtag elekezi na operesheni za kidijitali hutumika kuendesha kampeni hiyo.
-
Wall Street Journal: Nguvu ya Makombora ya Iran Yaweza Kuipatia Marekani na Washirika Wake Hasara Kubwa
Wall Street Journal yaripoti kuwa Iran ina takribani makombora 2,000 ya balistiki pamoja na mishale ya cruise na drones, yenye uwezo wa kusababisha hasara kubwa kwa maslahi ya Marekani na washirika wake katika Asia Magharibi, huku uwepo wa wanajeshi 40,000 wa Marekani ukiongeza changamoto za kiusalama.
-
Uchambuzi wa New York Times;
Je, , Beirut inaweza kuipokonya silaha Hezbollah ifikapo mwishoni mwa mwaka 2025?
Wachambuzi wanaonya kuwa ikiwa Beirut itaharakisha zoezi la kuipokonya silaha bila kupata mafanikio sambamba kutoka kwa Israel - kama vile kusitishwa kwa mashambulizi ya anga- hatua hiyo inaweza kuimarisha nafasi ya kisiasa na kijamii ya Hezbollah. Hii ni kwa sababu Hezbollah si kundi la kijeshi pekee, bali pia ni chama cha kisiasa chenye ushawishi mpana.
-
Baghdad yafuatilia kuongezeka kwa uwepo wa ISIS
Wasiwasi wa kiusalama nchini Iraq kuhusu shughuli za ISIS mpakani na Syria umeongezeka, licha ya hatua kali za kiusalama, huku kukiwa na maonyo ya kiintelijensia na ongezeko la tahadhari.
-
Utawala wa Kizayuni: Hezbollah imerejesha uwezo wake wa kijeshi katika sehemu kubwa ya majimbo ya mapigano (Mapambano)
Maafisa wa Israel wametoa tahadhari kwamba Hezbollah, kwa msaada wa kifedha kutoka Iran, imefanikiwa kurejesha uwezo wake wa kijeshi na sasa inachukuliwa kuwa tishio la kimkakati kwa Tel Aviv.
-
Daesh wabeba jukumu la shambulio dhidi ya doria ya wanamgambo wa Jolani
Daesh wametekeleza tukio la kushambulia doria inayohusiana na idara ya forodha ya Serikali ya Jolani na kuua watu wawili.
-
Kikundi cha “Abu Shabab” Kusini mwa Ukanda wa Gaza kiko katika hali ya kusambaratika
Kikundi cha wanamgambo kinachoitwa “Abu Shabab” kiko karibu kabisa kuvunjika baada ya kupoteza msaada wa anga kutoka kwa Israel na kushambuliwa kwa mashambulizi ya kulipiza kisasi kutoka kwa Harakati ya Hamas.