Main Title
24 Aprili 2024
Borrell: Uharibifu wa Israel huko Gaza unazidi uliofanywa katika miji ya Ujerumani katika Vita vya Pili vya Dunia
Mkuu wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya amesema kuwa vita vya Israel dhidi ya Gaza vimesababisha uharibifu mkubwa kwenye miji ya eneo hilo kuliko ule uliosababishwa na Vita vya Pili vya Dunia kwenye miji ya Ujerumani.
24 Aprili 2024
Rais Raisi: Israel ikifanya kosa jengine dogo haitabaki tena
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema katika kikao na wasomi wa jimbo wa Punjab nchini Pakistan kwamba iwapo utawala wa Kizayuni wa Israel utafanya kosa jengine dogo na kuivamia ardhi takatifu ya Iran, hali itakuwa tofauti kabisa na hakuna ajuaye kama utawala huo utabaki tena.
24 Aprili 2024
Msemaji wa Serikali ya Iran: Kuna Pengo kubwa kati ya viongozi wa Marekani na maoni ya umma
Msemaji wa Serikali ya Iran amesema, akizungumzia msaada mpya wa kifedha wa Marekani kwa utawala wa Kizayuni wa Israel, kwamba: Pengo kubwa lililopo kati ya watawala walioathiriwa na Uzayuni na maoni ya umma katika nchi za Magharibi haliwezi kukanushwa tena.
24 Aprili 2024
Sisitizo la Rais wa Iran kwamba Palestina ni suala kuu la Ulimwengu wa Wanadamu
Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza kwa mara nyingine tena kuwa kadhia ya Palestina ndilo suala kuu la Ulimwengu wa Wanadamu.
24 Aprili 2024
Kan'ani: Ukiukaji wa haki za binadamu nchini Marekani umeitia wasiwasi dunia
Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Iran amesema kuwa, ukiukaji wa kutisha wa haki ya kupiga kura, uhuru wa kusema na haki za binadamu huko Marekani unawatia wasiwasi mkubwa watu duniani.
24 Aprili 2024
Kiongozi wa Mapinduzi ya Kiislamu: Taifa la Iran halitasalimu amri mbele ya sera za mabavu
Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu amesema: Taifa kubwa na lenye historia ya miaka mingi la Iran halitasalimu amri mbele ya sera za kidhalimu na za kupenda kujitanua na litafika kwenye upeo mzuri wa mustakabali kwa kugeuza vikwazo kuwa fursa.
24 Aprili 2024
Kwa mara ya kwanza, Hizbullah yashambulia ndani kabisa ya ngome za Wazayuni tangu vilipoanza vita vya Ghaza
Hizbullah ya Lebanon imetangaza kuwa imefanya mashambulizi ya ndege zisizo na rubani dhidi ya vituo viwili vya kiejshi vya utawala wa Kizayuni wa Israel kulipiza kisasi cha mauaji ya wapiganaji wake wawili.
24 Aprili 2024
Mmarekani ambaye hana uraia wa Israel akiri kuua watu katika vita huko Gaza
Sami Benn, Myahudi raia wa Marekani, amekiri kwamba umeshiriki katika vita vya Israel kwenye Ukanda wa Gaza kwa muda wa miezi miwili na kuua Wapalestina, bega kwa bega na jeshi la Israel.
23 Aprili 2024
Sunak: Safari za kwanza za ndege kuelekea Rwanda za wanaotafuta hifadhi zitaanza baada ya wiki 10 hadi 12
Waziri Mkuu wa Uingereza, Rishi Sunak, ameahidi kwamba safari za kwanza za ndege za nchi hiyo za raia wa nchi mbalimbali wanaotafuta hifadhi zitaanza kuondoka Uingereza kuelekea Rwanda baada ya wiki 10-12.
23 Aprili 2024
Onyo jipya kuhusu kuingia NATO katika vita vya Ukraine
Viktor Orbán, Waziri Mkuu wa Hungary amesema katika taarifa kwamba viongozi wa Umoja wa Ulaya na Jumuiya ya Kujihami ya Kijeshi ya Magharibi (NATO) wanauchukulia mzozo wa Moscow na Kyiv kuwa ni wao na wala hawazingatii hatari ya kujihusisha na mzozo huo. Ameonya kuwa NATO inakaribia kutuma askari wake huko Ukraine.
23 Aprili 2024
Waandishi wakosoaji wa Israel wasusia tamasha la jumuiya ya PEN America
Tamasha ya Jumuiya ya Kalamu ya Marekani (PEN America) imefutwa kutokana na ukosoaji mkubwa wa waandishib walioalikwa katika sherehe hiyo dhidi ya jinai na uhalifu unaofanywa na Israel huko Gaza.
23 Aprili 2024
Chama cha Congress cha India chataka Modi achukuliwe hatua kwa matamshi yake ya dhidi ya Waislamu
Chama cha Indian National Congress, ambacho ndicho kikubwa zaidi cha upinzani nchini India, kimewasilisha ombi kwa Tume ya Uchaguzi kikitaka kuchukuliwa hatua dhidi ya Waziri Mkuu wa India, Narendra Modi, kwa kutoa matamshi ambayo Congress inasema "hayakubaliki kabisa" dhidi ya Waislamu nchini humo na yanakiuka sheria za uchaguzi.
23 Aprili 2024
Tume ya Haki za Binadamu ya Ulaya: Uingereza isitishe mpango wa kuwapeleka wahamiaji huko Rwanda
Tume ya Kutetea Haki za Binadamu ya Ulaya, imetoa wito kwa Uingereza kutupilia mbali mpango wake wenye utata wa kuwatuma waomba hifadhi nchini Rwanda.
23 Aprili 2024
Rais wa Iran asisitiza kukuza ushirikiano wa pande mbili na Pakistan
Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesisitiza udharura wa kukuza ushirikiano kati ya Tehran na Islamabad katika nyanja mbalimbali.
23 Aprili 2024
Safari ya Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Pakistan
Ziara ya siku mbili ya Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran nchini Pakistan inatathminiwa kuwa ni safari ya kihistoria ambayo inatarajiwa kufungua ukurasa na anga mpya ya uhusiano kati ya Tehran na Islamabad.
23 Aprili 2024
Raisi: Iran itaendelea kuunga mkono uhuru wa Syria
Rais wa Iran Ebrahim Raisi amesema Jamhuri ya Kiislamu itasimama kidete pamoja na Syria na itaendelea kuunga mkono uhuru wake na umoja wa ardhi yake.
23 Aprili 2024
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran akosoa ufuasi kipofu wa Ulaya kwa Marekani
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amekosoa uamuzi wa Umoja wa Ulaya wa kuiwekea Iran vikwazo vilivyo kinyume cha sheria, akisema kuwa watu wa Ulaya hawapaswi kufuata ushauri wa Marekani wa kuuridhisha utawala mtendajinai wa Israel.
23 Aprili 2024
Ndege za kivita za jeshi la Israel zashambulia makazi ya raia Ukanda wa Gaza
Ndege za kivita za utawala haramu wa Kizayuni Israel jana zilishambulia kusini kwa Ukanda wa Gaza na kubomoa nyumba kadhaa za raia katikati mwa Gaza na shule moja katika kambi ya wakimbizi ya al Bureij.
23 Aprili 2024
OIC yataka uchunguzi ufanyike kuhusu ‘uhalifu wa kivita’ wa Israel huko Khan Yunis, Gaza
Jumuiya ya Ushirikiano wa Kiislamu (OIC) imetoa wito wa kufanyika uchunguzi kuhusu uhalifu wa kivita wa Israel katika Hospitali ya Nasser huko Gaza ambapo mamia ya miili ya raia imeopolewa kutoka kwenye makaburi ya umati.
23 Aprili 2024
Walowezi wa Kizayuni wauhujumu Msikiti wa Al-Aqsa kutekeleza ibada za Pasaka
Makumi ya walowezi wa Kizayuni wamevamia Msikiti wa Al-Aqsa katika mji wa Quds (Jerusalem) siku ya Jumatatu chini ya ulinzi mkali wa wanajeshi wa utawala ghasibu wa Israel ambao unakalia eneo hilo kwa mabavu.