Main Title

source :
Jumatano

17 Aprili 2024

17:09:46
1452133

Ebrahim Raisi: Wazayuni wataelewa maana halisi ya majibu ya Iran

Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, iwapo Israel itafanya kosa jingine lolote dhidi ya Iran, basi Wazayuni na waungaji mkono wao wataelewa maana halisi ya majibu ya Jamhuri ya Kiislamu.

source :
Jumatano

17 Aprili 2024

17:09:20
1452132

Iran iliwasiliana na nchi za eneo katika kutekeleza Operesheni ya Ahadi ya Kweli dhidi ya Israel

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran anayehusika na masuala ya kisiasa amesema: Iran ilikuwa ikiwasiliana na nchi za eneo katika mchakato wa kutoa jibu kwa utawala wa Kizayuni na utekelezaji wa Operesheni ya Ahadi ya Kweli.

source :
Jumatano

17 Aprili 2024

17:08:47
1452131

Rais Raisi: Operesheni ya "Ahadi ya Kweli" ilikuwa hatua ya kiwango maalumu na ya kuwatia adabu tu Wazayuni

Rais Ebrahim Raisi wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema, Operesheni ya Ahadi ya Kweli ilikuwa hatua ya kiwango maalumu na ya kuutia adabu tu utawala wa Kizayuni na akasisitiza kwamba, endapo utawala huo utafanya uchokozi mdogo kabisa dhidi ya ardhi ya Iran utakabiliwa na jibu kali zaidi na la nguvu kubwa zaidi.

source :
Jumatano

17 Aprili 2024

17:08:20
1452130

Kujitetea kwerevu kwa Iran kwa ajili ya Gaza

Hatua ya Iran kujitetea kihalali dhidi ya shambulio la kichokozi la utawala wa Kizayuni katika ubalozi mdogo wake nchini Syria, ambayo ilifanyika kwa utaratibu wa hali ya juu na kupitia silaha tofauti za mashambulio, imekuwa na athari na matokeo ya kieneo na kimataifa angalau imepelekea wakaazi wa Gaza kupata usiku mmoja wa amani na utulivu.

source :
Jumatano

17 Aprili 2024

17:07:36
1452128

UN: Israel imeua wanawake 10,000 Gaza

Takriban wanawake 10,000 wameuawa huko Gaza tangu utawala haramu wa Israel uanzishe vita vya mauaji ya kimbari dhidi ya eneo hilo Oktoba mwaka jana.

source :
Jumatano

17 Aprili 2024

17:07:14
1452127

Wapalestina 16 wa Ukanda wa Ghaza wameuawa shahidi kwenye jela za utawala wa Kizayuni

Kamati inayoshughulikia masuala ya Wapalestina wanaoshikiliwa na walioachiwa huru kutoka kwenye magereza ya utawala wa Kizayuni wa Israel imetangaza kuwa, mateka 16 wakazi wa Ukanda wa Ghaza wameuawa shahidi wakiwa wanashikiliwa kwenye magereza ya utawala huo.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:30:53
1451872

Bunge la Marekani laionya Washington isijiingize kwenye vita vya kijeshi na Iran

Mkuu wa Kamati ya Kijasusi ya Bunge la Marekani amewaonya viongozi wa Washington kuhusu matokeo mabaya ya kujiingiza katika hatua yoyote ya kijeshi inayoweza kuchukuliwa dhidi ya Iran.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:30:27
1451871

Ramaphosa: Kama Israel haitodhibitiwa, vita vya Ghaza vinaweza kuenea ukanda mzima

Rais wa Afrika Kusini kwa mara nyingine ameonya kuhusu hatari ya vita vya Ghaza na kuendelea jinai za utawala wa Kizayuni dhidi ya watu wasio na hatia akisisitiza kuwa kama Israel haitodhibitiwa, basi vita hivyo vinaweza kuenea katika nchi zote za eneo hili.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:29:45
1451870

Russia yakumbwa na mafuriko; nyumba zaidi ya elfu 15 zazama majini

Maafisa wa Russia wa Idara ya Kukabiliana na Majanga ya Kimaumbile wameeleza kuwa idadi ya nyumba zilizozama kutokana na mafuriko nchini humo imepindukia 15,000.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:29:14
1451869

Mienendo ya chuki dhidi ya Uislamu yaongezeka nchini Ujerumani

Vyombo vya habari vya Ujerumani, vimenukuu ripoti zilizochapishwa na serikali ya nchi hiyo, na kuripoti kuwa uhalifu dhidi ya Waislamu nchini humo uliongezeka mwaka 2023 ikilinganishwa na miaka ya kabla yake.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:28:38
1451868

Trump, rais wa kwanza wa zamani Marekani kuhukumiwa katika kesi ya jinai

Kesi ya Donald Trump katika mashtaka ya jinai ilianza jana, Jumatatu, mjini New York na kumfanya kuwa rais wa kwanza wa zamani wa Marekani kufika mbele ya mahakama ya jinai kujibu mashtaka yanayohusiana na kulipa pesa kwa mwigizaji wa filamu za ngono ili kumnyamazisha na kumtaka afiche uhusiano wake wa kingono na mwanamke huyo.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:28:15
1451867

Kikao cha Baraza la Usalama: Uwanja wa makabiliano kati ya waungaji mkono wa Iran na Wamagharibi wanaounga mkono utawala wa Kizayuni.

Kikao cha dharura cha Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kujadili mashambulizi ya Iran ya kuuadhibu utawala wa Israel kilifanyika Jumapili jioni tarehe 14 Aprili, kikao ambacho kilibadilika na kuwa uwanja wa makabiliano kati ya nchi zinazounga mkono Iran na kambi ya Magharibi waitifaki wa utawala wa Kizayuni.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:27:25
1451866

Tehran yaitaka UN ilaani shambulio la Israel kwenye ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa lina wajibu wa kulaani shambulio la kigaidi lililofanywa na utawala wa Kizayuni wa Israel kwenye ubalozi mdogo wa Iran mjini Damascus, Syria.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:26:47
1451865

Abdollahian amwambia Guterres: Hatukuwa na njia nyingine isipokuwa kuiadhibu Israel

Waziri wa Mashauri ya Kigeni wa Iran amesema kuwa, operesheni ya jeshi la Iran dhidi ya maeneo ya kijeshi ya utawala ghasibu wa Israel imefanyika ndani ya fremu ya kujilinda na kwa mujibu wa sheria za kimataifa.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:26:06
1451864

Amir-Abdollahian: Iran haitoruhusu Israel kuhatarisha usalama wa ukanda huu

Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran amesema kuwa, Jamhuri ya Kiislamu ya Iran inaamini kwamba usalama na utulivu wa nchi za eneo hili zima ni muhimu sana kwake, bali ni sawa kabisa na usalama wake yenyewe na haitoruhusu utawala wa Kizayuni kuhatarisha usalama wa eneo hili kwa chokochoko zake.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:25:30
1451863

Ebrahim Raisi: Hatua yoyote dhidi ya Iran itapata majibu makali

Rais wa Jamhuri ya Kiislamu ya Iran amesema kuwa, hatua yoyote hata ndogo kiasi gani itakayochukuliwa dhidi ya manufaa ya Iran, bila ya shaka yoyote itapata majibu makali na ya kuumiza kwa wote watakaohusika na hatua hiyo.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:25:08
1451862

Mgogoro ulioanzishwa na utawala wa Kizayuni; matokeo ya utawala wa Netanyahu na baraza lake la mawaziri

Kanali ya 12 ya utawala wa Kizayuni imesema kwenye tovuti yake kwamba Netanyahu ni mwongo na kwamba ameuletea madhara makubwa ya kiusalama utawala ghasibu wa Israel kwa kushindwa kijeshi katika Ukanda wa Gaza, kuzusha migogoro mbalimbali katika eneo na kuwa leo hii utawala huo unakabiliwa na matatizo ya pande zote.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:24:44
1451861

Vyombo vya habari vyafichua jinai ya Wazayuni katika Hospitali ya al-Shifa huko Gaza

Vyanzo vya habari vimevichua na kuweka wazi jinai kubwa iliyofanywa na askari wa utawala wa Kizayuni wa Israel katika Hospitali ya al-Shifa huko Gaza baada ya kufukuliwa miili ya mashahidi wa Kipalestina waliouawa na kuzikwa na wanajeshi wa utawala huo haramu.

source :
Jumanne

16 Aprili 2024

18:24:02
1451860

Wazayuni wanakwepa kurejea maeneo wanayoishi kwa kuhofia mashambulio ya Hizbullah

Televisheni ya utawala wa Kizayuni wa Israel imefichua kuwa, sehemu kubwa ya Wazayuni wanaoishi kaskazini mwa ardhi za Palestina zinazokaliwa kwa mabavu na utawala wa Kizayuni, wanakwepa kurejea maeneo hayo wakihofia mashambulio ya Hizbullah ya Lebanon.

source :
Jumatatu

15 Aprili 2024

20:29:37
1451638

Russia yakosoa kimya cha Baraza la Usalama baada ya shambulio la Israel katika ubalozi mdogo wa Iran, Syria

Russia imekosoa hatua ya Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa ya kushindwa kuchukua hatua inayofaa baada ya utawala wa Israel kushambulia jengo la ubalozi mdogo wa Iran huko Damascus mji mkuu wa Syria.