27 Machi 2025 - 15:50
Source: Parstoday
Bahraini, ambaye alikuwa akizungumza katika kikao kilichofanyika katika Makao Mkauu ya Umoja wa Mataifa kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya Kupmabana

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje wa Iran, Esmaeil Baghaei amemkosoa vikali mkuu mpya wa Sera za Kigeni wa Umoja wa Ulaya, Kaja Kallas, kutokana na matamshi yake ya karibuni ya kuitaja Iran kama "tishio" wakati wa ziara yake ya karibuni katika maeneo ya Palestina yanayokaliwa kwa mabavu na Israel.

Akijibu swali la ripota wa IRNA leo Alkhamisi, Baghaei amesema kuwa, kauli ya Kallas "haina msingi wala mantiki, ya kinafiki, na si ya kuaminika. Amesema Umoja wa Ulaya unapaswa kushughulikia mauaji ya halaiki na uchokozi wa utawala wa Israel dhidi ya nchi za eneo hili badala ya kutoa madai ya "kinafiki" dhidi ya Tehran.

Kallas alidai karibuni kuwa Iran ni "tishio" kwa utulivu wa kieneo na kimataifa na kwamba Tehran haipaswi kamwe kuruhusiwa kupata silaha za nyuklia. Alitoa madai hayo yasiyo na msingi katika mkutano na waandishi wa habari mjini al-Quds akiwa na Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel,  Gideon Sa'ar, ambapo pia aliituhumu Iran kwa kuunga mkono Russia katika vita na Ukraine.

Baghaei amesema iwapo Mkuu wa Sera za Kigeni wa EU anajali sana utulivu na usalama wa kikanda, angelishughulikia masuala kama vile mauaji ya kimbari ya Israel huko Gaza, uvamizi wa (utawala huo haramu) wa mara kwa mara dhidi ya Lebanon na Syria, na ukaliaji wa mabavu wa maeneo ya Asia Magharibi.

Bahraini, ambaye alikuwa akizungumza katika kikao kilichofanyika katika Makao Mkauu ya Umoja wa Mataifa kwa mnasaba wa Siku ya Kimataifa ya Kupmabana

"Bi. Kallas, tofauti na watangulizi wake ambao walijaribu kutoa mtazamo wa muda mfupi katika kanuni za sheria za kimataifa wakati wa kutangaza misimamo ya Umoja wa Ulaya, anazungumza kwa ujasiri kwa namna ambayo, hata ikiwa inatokana na kutokuwa na uzoefu, anazidi kuharibu sura na uaminifu wa Ulaya mbele ya waangalizi wasio na upendeleo," amesema.

Baghaei amelaani sera za undumakuwili za Umoja wa Ulaya na kusisitiza kuwa, matamshi ya Kallas hayana msingi wala mantiki na madai yake ya kinafiki dhidi ya Iran hayana itibari.

342/

Your Comment

You are replying to: .
captcha