Sayyid Abbas Araqchi ameeleza masikitiko yake kuhusu ufahamu usio sahihi wa Marekani mkabala wa watu wa Yemen na wa kanda hii na kusisitiza kuwa: Wanasiasa wa Marekani wanapaswa kuelewa kwamba, chanzo kikuu cha ukosefu wa usalama katika eneo hili ni kuendelea hatua za mabavu na mauaji ya kimbari huko Palestina inayokaliwa kwa mabavu, na kwamba Marekani haiwezi kudai kurejesha uthabiti katika eneo kwa kuishambulia Yemen na kuwaua watu wasio na hatia wa nchi hiyo ambao kosa lao pekee ni kudhihirisha mshikamano na kuwaunga mkono wananchi wanaodhulumiwa wa Palestina.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Iran ameeleza haya katika mazungumzo na "Hans Grundberg", Mjumbe Maalumu wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa katika masuala ya Yemen, ambaye alifanya ziara hapa Tehran kwa ajili ya mazungumzo na mashauriano na viongozi wa Iran.
Mkuu huyo wa chombo cha diplomasia wa Iran amekosoa kutochukua hatua Baraza la Usalama la UN mkabala wa ukiukaji wa wazi wa hati na sheria za kimataifa unaofanywa na utawala wa Israel na Marekani na kusisitiza kuwa Umoja wa Mataifa unaopasa kuchukua hatua chanya haraka iwezekanavyo ili kusitisha uvunjaji na ukiukaji wa sheria unaofanywa na Marekani na Israel.
342/
Your Comment