23 Aprili 2025 - 23:38
Source: Parstoday
Russia yapendekeza kuanzisha kituo cha diplomasia ya chakula katika BRICS

Russia imependekeza kuanzishwa kituo maalumu cha diplomasia ya chakula ili kuimarisha ushirikiano wa kibiashara na usalama wa chakula miongoni mwa nchi wanachama wa kundi la BRICS.

Dmitry Bulatov Mkuu wa Muungano wa Taifa wa Russia wa Wauzaji Nje Bidhaa za Chakula amesema katika mahojiano na televisheni ya BRICS kuwa: Pendekezo la kuanzisha "Kituo cha Diplomasia ya Chakula" limetolewa ndani ya mfumo wa Kamati ya Kitaifa ya Utafiti ya BRICS ili kuratibu utekelezaji wa maamuzi yanayohusiana na kupanua ubadilishanaji wa bidhaa za chakula   kati ya wanachama wa kundi hilo. 

Bulatov amesema: Kituo cha Russia cha Diplomasia ya Chakula kinaweza kuwa na nafasi chanya katika kuhakikisha  biashara ya kimataifa inakuwa endelevu.

"Upo ulazima kwa wataalamu wa nchi za BRIBS kutayarisha hati ya kimataifa ya maadili katika masoko ya chakula ili kutumika kama mfumo wa pamoja kwa nchi zinazofanya biashara ya kimataifa ya chakula," amesema Dmitry Bulatov Mkuu wa Muungano wa Taifa wa Russia wa Wauzaji Nje Bidhaa za Chakula. 

Bulatov pia amesisitiza kuhusu nafasi kuu ya Russia katika kudhamini usalama wa chakula duniani na kusema nchi hiyo ni ya kwanza duniani katika mauzo ya ngano, na ni miongoni mwa nchi wasambazaji wakubwa wa nafaka duniani.

342/

Your Comment

You are replying to: .
captcha