Main Title

source : Parstoday
Jumatano

16 Novemba 2022

17:18:22
1323738

Wademokrati wapigania kupitisha sheria ya ndoa za jinsia moja kutambuliwa rasmi Marekani

Kiongozi wa Wademokrati waliowengi katika Seneti ya Marekani Chuck Schumer ametangaza kuwa Seneti itaupigia kura mswada wa kuunga mkono ndoa za watu wa jinsia moja wiki hii baada ya kufikiwa makubaliano kati ya wajumbe wa Baraza la Wawakilishi la nchi hiyo.

Tangu mwaka 2015, Mahakama Kuu ya serikali kuu ya Marekani ilitoa hakikisho la kutambuliwa ndoa za watu wa jinsia moja. Lakini baada ya mahakama hiyo kubadilisha ghafla mtazamo yake juu ya uavyaji mimba, ulizuka wasiwasi mkubwa kwa watetezi wa maingiliano ya kimwili ya watu wa jinsi moja kwamba haki hiyo pia itapotea.Katikati ya Julai mwaka huu, Baraza la Wawakilishi la Marekani lilipitisha sheria ya kuunga mkono ndoa za jinsia moja nchini kote, ambapo wawakilishi wote wa chama cha Democrat na 47 wa Republican waliunga mkono hati ya sheria hiyo. Hata hivyo wawakilishi wapatao 160 wa Republican walipinga uamuzi huo.Tokea wiki chache zilizopita, mashauriano yamekuwa yakiendelea ndani ya baraza la Seneti kuhakikisha unapatikana uungaji mkono wa angalau maseneta kumi wa chama cha Republican kwa hati ya sheria hiyo, ambao unahitajika ili kuweza kuidhinishwa.

Siku ya Jumatatu, kundi la maseneta kutoka pande zote mbili lilitangaza kuwa makubaliano yamefikiwa juu ya suala hilo.Chuck Schumer amesema, utaratibu wa kwanza wa upigaji kura kuhusiana na hati ya sheria hiyo utafanyika leo Jumatano. Schumer ameutaka mrengo wa upinzani wa kihafidhina uunge mkono mswada huu, ambao kwa mtazamo wake amesema ni "muhimu sana".Wamarekani wengi wakiwemo wafuasi wa chama cha Republican wanaunga mkono kuruhusiwa kisheria ndoa za watu wa jinsia moja, lakini wengi wa wafuasi wa kidini wa mrengo wa kulia wa chama hicho wanapinga suala hilo.../


342/