Droni
-
Hezbollah Yaongeza Mashambulizi ya Droni, Makamanda wa Israel Walengwa Kusini mwa Lebanon
Hezbollah imeripotiwa kuanzisha kampeni ya kulenga makamanda waandamizi wa Israel kusini mwa Lebanon kwa kutumia droni za upelelezi na mashambulizi, huku ving’ora vya tahadhari vikisikika zaidi ya mara 25 kaskazini mwa Israel kutokana na makombora na droni zilizorushwa kutoka Lebanon.
-
Israel Yakiri Kushindwa Kukabiliana na Droni za Muqawama wa Lebanon
Jeshi la Israel limekiri kuwepo kwa hitilafu katika mifumo yake ya onyo dhidi ya droni za FPV zinazotumiwa na Muqawama wa Hezbollah, huku ripoti zikieleza kuwa teknolojia mpya ya droni hizo zinazoongozwa kwa “fiber-optic” imeongeza hofu na changamoto kubwa kwa vikosi vya utawala huo katika medani za mapambano.
-
Urusi Yatengeneza Njiwa-Droni Wenye Chipu za Ubongo
Bio-drones za Nairi Group zazua hofu za kijeshi kwa teknolojia ya udhibiti wa neva
-
Ukraine Yashambulia Makaazi ya Putin kwa Ndege Droni 91 / Trump Ashtuka
Ikulu ya Kremlin jioni ya Jumatatu ilitangaza kuwepo kwa mawasiliano ya simu kati ya marais wa Urusi na Marekani, na kubainisha kuwa Rais wa Marekani, Donald Trump, alishtushwa na shambulio la ndege zisizo na rubani (droni) la Ukraine dhidi ya makaazi ya Rais wa Urusi, Vladimir Putin.
-
Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Iran Lafichua Droni Mpya ya Kujitoa Mhanga ya Kasi ya Juu imayoitwa: “Hadid-110 | Hadid yaani: Chuma
Hadid-110 ilizinduliwa kwa kutumia mfumo wa reli unaosaidiwa na roketi, hali inayoiwezesha kufikia kasi ya juu mara baada ya kurushwa. Muundo wake wa kisasa unaojumuisha injini ndogo ya jet na umbo lenye pembe maalumu (low-observable faceted design) umeundwa mahsusi ili kupunguza uwezekano wa kugunduliwa na mifumo ya ulinzi wa anga.
-
Jeshi la Israel ladaiwa kumuua “Muhammad Akram Arabiyeh” mwanachama wa Kikosi cha Rizwan cha Hezbollah
Kwa mujibu wa vyanzo vya Kizayuni, katika kuendeleza uvamizi wake ndani ya ardhi ya Lebanon na mashambulizi dhidi ya wapiganaji wa muqawama, mwanachama wa Kikosi Maalumu cha Ridhwan cha Hezbollah ameuawa shahidi katika shambulizi la anga lililofanywa na Israel katika eneo la al-Qulay‘a, kusini mwa Lebanon.
-
Italia na Hispania Zimetuma Manowari za Kivita kwa ajili ya Kulinda Msafara wa Meli za Sumuud
Kufuatia mashambulizi ya ndege zisizo na rubani (droni) dhidi ya msafara wa kimataifa wa Sumuud (Jina la Msafara), ambao unalenga kupeleka misaada ya kibinadamu kwa Gaza na ulikuwa ukisafiri katika maji ya kimataifa, Italia na Uhispania zimetuma meli zao za kivita ili kuhakikisha usalama wa msafara huo. Hatua hii imechukuliwa baada ya kulaaniwa kwa kiwango kikubwa kwa mashambulizi hayo dhidi ya meli zisizo za kijeshi, ambayo yamechukuliwa kuwa ni uvunjaji wa sheria za kimataifa.
-
Marekani Yazindua Droni ya LUCAS ikiiga moja kwa moja Droni ya Shahed-136 ya Iran
Fikra hii ya kutengeneza Droni ya LUCAS imetokana na mshangao mkubwa ilioupata Marekani kutoka kwenye Droni Shahid - 136 ya Iran na uwezo wake katika Uwanja wa Kivita, kiasi kwamba Marekani ikaona Iran imepiga hatua kubwa katika masuala ya teknolojia ya Kuzalisha zana za Kivita na za gharama nafuu. Hilo liliifanya Marekani kuwaza kukopi Droni hiyo ya Iran hatimaye kuja na Droni yao waliyoiita LUCAS.
-
Iran | Ulinzi wa Anga: "Tumepambana na ndege za Kijeshi na Droni 130 hadi leo asubuhi
Katika Mapambano hayo, dhidi ya ndege za kivita na ndege zisizo na rubani (Droni) aina ya "Hermes", "Heron" na ndege za kujilipua aina ya "Harop", walifanikiwa kuziharibu na kuziangusha katika maeneo mbalimbali ya nchi.